Advertisements

Monday, July 18, 2016

RAIA WA AFRIKA KUSINI AFARIKI DUNIA MLIMA KILIMANJARO

 Raia wa Afrika Kusini waliopanda Mlima hivi karibuni kwa lengo la kuchangisha fedha kwa ajili ya kununua taulo za kusaidia watoto wa kike.aliyechuchumaa mbele (mwenye kofia) Gugu Zulu  ndiye anatajwa kufariki Dunia wakati akielekea Kileleni.
 Gugu Zule (Kulia) akiwa na Richard Mabaso muda mfupi kabla ya kuanza safari ya kupanda Mlima Kilimanjaro.
Gugu Zulu akiwa katika lango la Marangu akipata picha na mmoja wa washiriki wa safari hiyo muda mfupi kabla ya kuanza kupanda Mlima Kilimanjaro.

 Gugu Zulu (kushoto) akiwa na rafiki yake muda mfupi kabla ya kuanza safari ya kupanda Mlima Kilimanjaro katika kampeni ijulikanayo kama Trek4Mandela ikiwa na lengo la kchangisha fedha kwa ajili ya kunua taulo za watoto wa kike pamoja na kusherehekea kumbukumbu ya kuzaliwa kwa baba wa taifa la Afrika Kusini ,Nelson Mandela. 

Na Dixon Busagaga wa Michuzi Blog,Kanda ya Kaskazini.


Ra ia    wa    Afrika    ya    Kusini    Guguleth    Mathebula    Zulu    (38)    aliyefika    nchini    kwa    ajili    utalii    wa    kupanda    Mlima    Kilimanjaro    amefariki    leo    tarehe    18.7.2016    baada    ya    kupatwa    na    tatizo    la    kushindwa    kupumua    kwenye    mwinuko    wa    juu    mlimani.     

 Shirika    la    Hifadhi    za    Taifa    nchini    kwa    kushirikiana    na    mamlaka    mbalimbali    za    serikali    zinaendelea    na    uratibu    wa    kurejesha    mwili    wa    marehemu    nchini    Afrika    ya    Kusini    kwa    ajili    ya    taratibu    za    maziko.   

Zulu    alifika    nchini    na    kuanza    kupanda    Mlima    Kilimanjaro    tarehe    14.7.2016        kwa    ajili    ya    kuenzi    jitihada    za    Rais    wa    Kwanza    wa    Afrika    ya    Kusini        Nelson    Mandela    za    kusaidia    familia    maskini    nchini    Afrika    ya    Kusini,    hususani    kuwapatia    mahitaji    muhimu    watoto    wa    kike    ambao    hawana    uwezo    wa    kupata    mahitaji    muhimu.      

Hii    ni    mara    ya    pili    kwa    watalii    kutoka    Afrika    ya    Kusini    kupanda    Mlima    Kilimanjaro    kwa    ajili    ya    kuenzi    juhudi    za    Mandela    katika    kusaidia    jamii    ya    watoto    wa    kike    kupitia    kampeni    maalum    ya    kupanda    Mlima    Kilimanjaro. 

       Imetolewa    na    Idara    ya    Mawasiliano    Hifadhi    za    Taifa    Tanzania    
S.L.P    3134    
Baruapepe: dg@tanzaniaparks.go.tz    
Wavuti:    www.tanzaniaparks.go.tz    
18.07.201

1 comment:

Anonymous said...

inasikitisha na ukiangalia tena na hizo picha zake..R.I.P