Advertisements

Wednesday, July 27, 2016

TANZANIA YAZIDI KUPAA MATUMIZI YA SIMU ZA MIKONONI



 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof Makame Mbalawa akizungumza kwenye Mkutano wa siku tatu ( Julai 26-28)  unaoendelea jijini Dar es Salaam ukifahamika kama  2016 Mobile 360 Series – Africa  ukihusisha wadau mbalimbali wa mawasiliano ya simu za mikononi.
 Mkurugenzi Mkuu wa GSMA Bw Mats Granryad, akizungumza kwenye mkutano huo.



 Mkurugenzi wa GSMA Afrika Bw Mortimer Hope akizungumza kwenye mkutano huo.
 Baadhi ya washiriki wa Mkutano huo. 

Tanzania ni miongoni mwa mataifa manane barani Afrika ambayo yana soko kubwa la simu za mikononi, ripoti  mpya ya utafiti  iliyozinduliwa jana jijini Dar es Salaam imebainisha.
 
Kwa mujibu wa ripoti hiyo  ijulikanayo;  ‘Uchumi wa simu za mikononi: Afrika 2016’ iliyozinduliwa  kwenye Mkutano wa siku tatu ( Julai 26-28)   unahofahamika kama  2016 Mobile 360 Series – Africa  ukihusisha wadau mbalimbali wa aina hiyo ya mawasiliano, Tanzania  imeungana na mataifa ya Nigeria na Ethiopia ambayo  kwa utatu wao yanachukua zaidi ya theluthi moja  ya soko la aina hiyo ya mawasiliano barani Afrika.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo zaidi ya  watu nusu bilioni barani Afrika kwa sasa wamejiunga  na huduma ya simu za mikononi  huku kukiwa na idadi kubwa ya watumiaji wa aina hiyo ya mawasiliano wanaohamia kwenye huduma ya internet inayopatikana kwenye simu zao, utafiti mpya uliofanywa na na Umoja wa wadau wa Mawasiliano ya simu za mikononi  Duniani  ujulikanao kama GSMA umebaini.
Ripoti hiyo pia iliangazia mchango wa sekta ya mawasiliano ya simu hizo kiuchumi, ikiwemo ajira, ufadhiri kwa umma (Public Funding) pamoja na mchango wa mawasilian hayo katika ukuaji wa digitali na ushirikishwaji wa kifedha.
“Zaidi ya watu nusu bilioni barani Afrika kwa sasa wamejiunga na huduma ya simu za mikononi, hatua ambayo si tu inawaunganisha bali pia inatoa fursa kwao kuweza kupata huduma nyingine kama vile huduma za afya, utambuzi wa kidigitali na huduma za kifedha,’’ alibainisha Mats Granryad, Mkurugenzi Mkuu wa GSMA. “Uhamiaji wa ghafla kwenda kwenye matumizi ya internet ya simu miongoni mwa watumiaji  inatoa fursa mpya kwa watumiaji, biashara, serikali na kukuza mzunguko ambao mwaka jana uliongeza zaidi ya dola bilioni 150 kwenye uchumi wa bara la Afrika,’’
Uwekezaji kwenye mtandao (Network) na simu za kisasa (Smartphones) kunachochea uhamiaji zaidi kwenda kwenye matumizi ya internet ya simu.

No comments: