Advertisements

Sunday, July 17, 2016

WANAJESHI 2,839 WAKAMATWA BAADA YA JARIBIO LAO LA MAPINDUZI KUSHINDWA


Waziri Mkuu wa Uturuki Binali Yildirim amesema wanajeshi 2,839 wakiwemo maafisa wa ngazi za juu, wamekamatwa baada ya jaribio la mapinduzi lililozimwa.
Miongoni mwa wanaoshikiliwa wamo majenerali wawilia wa jeshi, kwa mujibu wa vyombo vya habari vya nchi hiyo.

Waziri Mkuu huyo ameliita jaribio hilo la mapinduzi kama doa jeusi katika demokrasia, na kueleza kuwa raia 161 wameuwawa na wengine 1,440 wamejeruhiwa.
Raia wenye hasira wakiwadunda wanajeshi baada ya kuwadhibiti na kuzima jaribio lao la mapinduzi
    Mwanajeshi aliyedhibitiwa na raia akipigwa ngumi nzito ya shavuni na mmoja wa raia





No comments: