Advertisements

Wednesday, August 10, 2016

BUZWAGI YAKABIDHI SHULE MPYA NA NYUMBA ZA WALIMU KWA SERIKALI WILAYANI KAHAMA.

Meneja Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi Asa Mwaipopo akifafanua jambo kwa wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Kahama wakati wa ziara ya kupokea miradi ya maendeleo.
Mkuu wa Wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu (aliyeweka mkono kwenye mfuko wa suruali) akiwa na wajumbe wengine wa kamati ya ulinzi na Usalama wa wilaya ya Kahama walipofanya ziara katika mgodi wa Buzwagi wa kukabidhiwa miradi ya maendeleo. 

Meneja Mkuu wa Mgodo wa Buzwagi Asa Mwaipopo akieleza jambo kwa wajumbe wa kamati ya ulinzi na Usalama wakiongozwa na Mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu.
  Kifaa maalumu cha kupoza umeme ambacho kitatumika kupeleka umeme katika mji wa Kahama na kungunguza tatizo la kukosekana kwa umeme kikiwa kimefungwa katika kituo cha Umeme cha mgodi wa Buzwagi.
 Meneja Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi Asa Mwaipopo (Mwenye kofia ya blue) akitoa maelezo kwa mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu (mwenye kofia ya kaki) wakati wa makabidhiano ya madarasa ya shule mpya ya msingi ya Budushi, wengine katika picha ni mbunge wa kahama mjini Mhe.Jumanne Kishimba na Mwenyekiti wa halmashauri ya mji Kahama Mhe.Abel Shija. 
  Mkuu wa wilaya Kahama Fadhili Nkurlu na Mbunge wa Kahama Mhe.Jumanne Kishimba wakizindua majengo ya shule mpya ya Budushi iliyojengwa kwa ufadhili wa mgodi wa Buzwagi.
Mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu na Mwenyekiti wa kijiji cha Budushi wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya uzinduzi wa majengo na nyumba moja ya walimu katika shule hiyo.
Mkuu wa wilaya ya Kahama, Fadhili Nkurlu (mwenye kofia ya kaki) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Mgodi wa Buzwagi na Watendaji wa Kata ya Mwendakulima
Moja ya majengo ya madarasa yaliyojengwa katika Shule ya Msingi Budushi chini ya ufadhili wa Mgodi wa Buzwagi.
Mkuu wa wilaya ya Kahama, Fadhili Nkurlu akiteta jambo na baadhi ya viongozi wa kata ya Mwendakulima.

Na Dixon Busagaga wa Michuzi Blog kanda ya Kaskazini.

Kampuni ya uchimbaji wa madini ya Acacia kupitia Mgodi wake wa Buzwagi uliyoko wilayani Kahama, katika mkoa wa Shinyanga, umekabidhi kwa uongozi wa katika Halmashauri ya mji wa Kahama majengo ya shule mpya ya msingi Budushi yenye madarasa sita, ofisi ya walimu na nyumba moja ya walimu yenye uwezo wa kuishi familia mbili.
Akikabidhi madarasa hayo kwa mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu, Meneja Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi mhandisi Asa Mwaipopo amesema ujenzi huo umefadhiliwa na Mgodi wa Buzwagi kwa zaidi ya shilingi milioni mia nne na themani kupitia mfuko wa Acacia Maendeleo Fund, ambao umelenga kuwapunguzia adha wanafunzi wa eneo hilo la Budushi na maeneo yanayozunguka eneo hilo kuondokana na adha ya kutembea mwendo mrefu kwenda shule.
Aidha, Meneja mkuu huyo wa Mgodi wa Buzwagi alikabidhi pia nyumba mbili za kisasa za walimu zenye uwezo wa kuishi familia nne kwa shule ya msingi Mwime hatua ambayo amesema kuwa itasaidia katika kupunguza tatizo la nyumba kwa walimu kwa shule hiyo. Nyumba hizo ambazo zimejengwa kwa kutumia teknolojia ya Tofali za kufungamana zimegharimu shilingi milioni mia mbili arobaini na nane (248,126,000/=)
Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Kahama Mh. Fadhili Nkurlu aliyepokea miradi hiyo ameupongeza uongozi wa Mgodi wa Buzwagi kwa jitihada ambazo wamekuwa wakizifanya katika kuhakikisha wanashirikiana na jamii katika kutekeleza miradi ya Maendeleo”
Akizungumza kwa niaba ya halmashauri ya mji wa Kahama Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Abel Shija ameupongeza uongozi wa Mgodi na kuahidi kuendelea kushirikiana nao katika kuiletea Jamii Maendeleo.

                                                                     Mwisho.

No comments: