Advertisements

Thursday, August 4, 2016

DC SOPHIA MJEMA AKUTANA NA WAZEE WA CCM ILALA

Mkuu wa wilaya ya Ilala Mh. Sophia Mjema akizungumza kwa unyenyekevu mbele ya Wazee wa CCM wilaya ya Ilala wakati alipokutana nao ili kujitambulisha na kufahamiana nao baada ya kuanza kazi kama mkuu wa wilaya hiyo, Aliwaomba wazee hao kushirikiana naye bega kwa bega na kumpa ushauri wa kila mara ili aweze kutekeleza majukumbu yake ya kuwaletea maendeleo wananchi wa wilaya hiyo na kufanikisha mipango ya Rais Mh. Dk John Pombe Magufuli ili kutekeleza kwa ufanisi ilani ya uchaguzi ya CCM, Katika picha kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ilala Ndugu Asaa Simba , Mkutano huo ulifanyika kwenye ofisi za CCM wilaya ya Ilala.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ilala Ndugu Asaa Simba akimkaribisha mkuu wa wilaya ya Temeke Mh. Sophia Mjema ili kuongea na wazee wa CCM wilaya ya Ilala.
Mkuu wa wilaya ya Ilala Mh. Sophia Mjema akimsikiliza Katibu wa CCM wilaya ya Ilala Bw. Kafuge Joel alipokuwa akizungumza mambo kadhaa kabla ya umkaribisha mwenyekiti wake ili kumkaribisha mkuu wa wilaya.
Baadhi ya wazee wa CCM wilaya ya Ilala wakiwa katika mkutano huo uliowakutanisha na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mh. Sophia Mjema.
Baadhi ya wazee wa CCM wilaya ya Ilala wakiwa katika mkutano huo uliowakutanisha na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mh. Sophia Mjema.

No comments: