Mzee Yusuf amesisitiza kuwa ameachana rasmi na muziki na hana maskhara na
hatua aliyoichukua ya kumtumikia Mwenyezi Mungu.
Akiongea leo, Mzee alisema sanaa pekee atakayoshiriki ni ile itakayohusiana na dini
yake ya Kiislam kama vile kuandaa nyimbo za kaswida na kucheza filamu za
maadili ya dini.
“Nimeshatengeneza
nyimbo mbili za kaswida, lengo langu ni kukamilisha albam pamoja na video yake
na baada ya hapo nitafanya mkutano na waandishi wa habari na kuweka wazi
malengo yangu nje ya muziki wa kidunia,” alisema Mzee Yusuf.
Mzee
aliyekuwa mtunzi, mwimbaji na mmiliki wa Jahazi Modern Taarab, amesema
ameshawaambia viongozi waliobakia kuwa wasiendelee kutumia jina lake na picha
zake kwenye matangazo ya bendi kwa sababu kufanya hivyo ni kuwaongopea watu.
“Najua yako
matangazo ambayo yameshatengenezwa kwaajili ya maonyesho mengi yajayo
yakihusisha jina langu, sina tatizo na hilo lakini kwa matangazo mapya
yatakayofanywa kuanzia sasa sitahitaji jina na picha zangu zitumike,”
alifafanua Mzee Yusuf na kongeza kuwa hiyo ni hatua ya kwanza na kwamba kuna
mambo mengine ya msingi yatafuata baadae.
Akizungumzia
namna anavyojiskia baada ya kuamua kuzama kwenye ibada na kuachana na muziki,
Mzee Yusuf alisema: “Kwa kweli najiskia raha sana, sasa ni nina wingi wa
utulivu na amani. Namuomba Mwenyezi Mungu aendelee kuniongoza kwenye njia ya
haki.
“Hii ni vita
kubwa, kuishinda vita hii sio jambo la mchezo, namuomba Mungu aniepushe na
vishawishi vitakavyokuja mbele yangu. Sitaki kurejea kwenye muziki.”
Aidha, Mzee
Yusuf amesema si kweli kuwa amebadili dhehebu kama ilivyoripotiwa na baadhi ya
watu kuwa ameijiunga na dhehebu la Answar Sunna.
No comments:
Post a Comment