Advertisements

Tuesday, August 9, 2016

NI MKOANI KATAVI,MWIGULU NCHEMBA ATOA ONYO KALI KWA WAKIMBIZI WANAOHIFADHI WAHALIFU NA WANAOFANYA UBAGUZI

Waziri wa Mambo ya ndani akisikiliza ripoti ya Mkoa wa Katavi kutoka kwa kaimu Mkuu wa Mkoa huyo ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Mpanda.Askari wa Jeshi la polisi kwa idara zote wakiimba wimbo wa maadili tayari kwa kumsikiliza Mh:Mwigulu Nchemba wilaya ya Mpanda Mjini.Waziri wa mambo ya ndani akiangalia tofali zilizoandaliwa kwaajili ya ujenzi wa makazi ya askari mpanda mjini.Kamati ya Usalama wa Mkoa wa
Katavi wakimuonesha Mh:Mwigulu Nchemba sehemu iliyobakia katika ujenzi wa ukumbi wa mikutano wa jeshi la polisi.Mwigulu amepongeza hatua hizo na kuahidi kuhakikisha anawasaidia kukamilisha hatua iliyobakia haraka iwezekanavyo.Mwigulu Nchemba akiwasili kwenye Gereza la mpanda kwaajili ya kusikiliza kero za wafungwa.Mwigulu Nchemba akiwasili ofisi za UNHCR zilizopo Shimano umbali wa KM 200 kutoka Kigoma Mjini.Mwigulu akipata maelekezo kutoka kwa Mkuu wa Makazi wa kambi ya Katumba alipotembelea kukagua uhakiki wa wakimbizi unaoendelea katika kambi hiyo.Mwigulu akiondoka kambi ya Katumba mkoani Katavi."Nyumba ya askari inapaswa kuwa na hadhi kama hii,uwezo tuna na nia tunayo ya kuhakikisha askari wetu wanakaa kwenye makazi bora"Mwigulu Nchemba akitoka kukagua nyumba ya kisasa kukaa askari polisi katika wilaya pendekezwa ya Tanganyika.Nyumba imejengwa kwa ushirikiano kati ya wananchi,UNHCR na Serikali ya Tanzania.
Waziri wa mambo ya ndani ya Nchi,Mh:Mwigulu Nchemba akiagana na wakimbizi waliopo kambi ya Shimano iliyopo Mkoa wa Rukwa mara baada ya kuzungumza nao.

Katika ziara yake kwenye kambi ya wakimbizi ya Katumba na Shimano,Mwigulu Nchemba amezungumza na wakimbizi hao ambao wale wa Katumba walipewa Uraia mwaka 2009 na wa Shimano bado hawajapewa Uraia.Akizungumza nao katika hali ya kusikitisha,kuna baadhi ya watu tumewapa Uraia lakini matendo yao yanachafua hali ya usalama wetu,miongoni mwenu kunawanaojihusisha na wizi,uhalifu wa kutumia silaha,kuhifadhi waovu na kufanya vitendo vya kibaguzi kwa misingi ya maeneo mnayotoka.
Mbaya zaidi,kunawakimbi waliopewa uraia hapa nchi wanawatenga watanzania kwamba hawawezi kushirikiana nao.Natoa onyo kwa wote wanaofanya vitendo vya kibaguzi na kihalifu,Tanzania inaishi kwenye misingi ya Umoja,mshikamano na Ushirikiano wa hali ya juu bila kubaguana.Hivyo hatutakuwa tayari kwa watu wachache kuleta tabia mbovu ambazo hatujawahi kuziishi na tunaomba kila siku tusije kuziishi."anasema mwigulu.
Picha/Maelezo na Sanga Festo Jr. 

No comments: