Advertisements

Saturday, August 20, 2016

SUMATRA YASEMA HAKUNA USAFIRI UTAKAOSITISHWA

MAMLAKA ya Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) imewatoa hofu Watanzania kuhusu taarifa za kutokuwepo kwa huduma ya usafiri wa mabasi kwenda mikoani kuanzia Jumatatu na kusema kuwa inafuatilia kuhakikisha kuwa huduma hiyo inatolewa wakati wote.
Pia, imesema maazimio yaliyotolewa na Chama cha Wamiliki wa Mabasi (Taboa) kuhusu kufanyika kwa ukaguzi wa mabasi yote yaendayo mikoani Agosti 22, mwaka huu, usitishwe na kuwataka kutoa huduma hiyo hadi utaratibu maalumu utakapopatikana.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mkuu wa Sumatra, Gilliard Ngewe, alisema Taboa ilipeleka maazimio matatu yanayohusu ukaguzi wa magari unaolenga kuimarisha usalama na ubora wa huduma wanazotoa kwa jamii.
Ngewe alisema mamlaka hiyo inakamilisha utaratibu huo wa kukagua magari pamoja na madereva na kwamba wanahitaji kuzungumza na taasisi inazoshiikiana nazo, ikwemo Kikosi cha Usalama Barabarani.
“Maazimio haya ni mazuri na yanalenga kutoa huduma bora lakini hatuwezi kuanza ukaguzi Agosti 22 kwa kuwa tunahitaji vifaa kwa ajili ya kufanya ukaguzi huo na kujua ni mabasi yapi yataanza ukaguzi na yatakayofuata,’’ alisema Ngewe na kuongeza kuwa, wamiliki wa mabasi hayo pamoja na madereva wanatakiwa kufuata masharti ya leseni walizopewa kwa kusafirisha abiria hadi utaratibu rasmi wa ukaguzi utakapotolewa.
Hata hivyo, alisema wananchi hawana budi kuondoa hofu ya kukosa usafiri kwakuwa hakuta utakaositishwa ili kupisha ukaguzi huo.

No comments: