RSM, Mtandao wa Kimataifa katika
ukaguzi wa mahesabu na tathmini za kodi, umesherehekea madhimisho
tano ya kila mwaka ya Siku Maalumu Duniani ya RSM—kwa kuchangia madawati
kwa shule mbalimbali za Dar es Salaam.
Mchango wa RSM, Mtendaji Mkuu wa RSM
Afrika Mashariki, Bi. Lina Rantasi alisema kuwa timu ya RSM imedhamiria
kusaidia jitihada za Serikali za kuokoa maisha na kuendeleza elimu.
Bi. Ratansi aliendelea kusema,”Kumekuwa
na wito mwingi wa kuchangia madawati, Na sisi hatutaki kubaki nyuma, ndo maana
tumetoa madawati 50 (3, 750, 000) ili kusaidia watoto wasika chini tena.”
Amesema madawati utasaidia
kuongeza uwezo na akili za watoto katika masomo, hivyo kuongeza ufaulu, kwa
sababu “motto akikaa chini hata ufahamu wake unakuwa mdogo.
Akipokea madawati hayo kwa niaba ya
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Kamati ya Madawati-Mkoa wa Dar es
Salaam, Hamid Abdul Rahaman, amesema mchango wa RSM utasaidi kukuza sekta ya
elimu, na kuwapongeza Mtandao wa RSM kwa kuunga mkono kampeni ya kitaifa ya
kuziwezesha shule kuwa na madawati ya kutosha.
No comments:
Post a Comment