Advertisements

Monday, September 19, 2016

TANZANIA IMEONYESHA UTASHI WA KISIASA KUWEKEZA KATIKA ELIMU-BAN KI MOON

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, akizungumza wakati wa uzinduzi wa Ripoti ya Kamisheni ya Kimataifa kuhusu“ Kizazi kinachojifunza: Uwekezaji katika elimu kwa dunia inayobadilika”. hafla ya uzinduzi wa ripoti hiyo ambayo imeandaliwa na Makamishna 27 akiwamo Rais Mstaafu wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete ilifanyika siku ya jumapili Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa.
.Mwenyekiti wa Kamisheni na Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu kuhusu Elimu, Waziri Mkuu Mstaafu wa Uingereza,Bw. Gordon Brown akiwasilisha mbele ya washiriki taarifa fupi ya kilichomo kwenye ripoti ya kamisheni yake ambapo suala kubwa lililositizwa katika ripoti hiyo ni uwekezaji wa raslimali fedha kwenye elimu.
Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akichangia na kuongoza majadiliao kuhusu kipengele cha ujumuishi katika elimu, ambapo alisema ripoti hiyo imeainisha mikakati na mipango ya kuwafikia makundi ya jamii yanayoishi katika mazingira magumu kama vile wakimbizi, wasichana, watoto wa mitaani, watoto walio katika ajira na watoto wanaobaguliwa.
4. Sehemu ya washiriki wa hafla ya uzinduzi wa Ripoti kuhusu Elimu
Kwa taarifa na picha zaidi bofya
Rais mstaafu Kikwete akiwa na Makamishna wenzie kushoto ni aliyekuwa Kamishna wa Umoja wa Ulaya Bw. Jose Manuel Barroso na Rais Mstaafu wa Mexico Bw. Felipe Calderon
Rais Mstafu Kikwete akisalimiana na Bibi. Ngozi Okonjo- Iwela Waziri wa zamani wa Fedha wa Nigeria.
Kamishna Teopista Birungi Mayanja kutoka Uganda ambaye katika mchango wake alisisitiza sana ushirikishwaji wa walimu katika mchakato mzima wa kuifanyia mageuzi sekta ya elimu ili iweze kuwafikia watoto wote. akasisitiza pia umuhimu wa walimu kuachwa watekeleze majukumu yao ya ualimu pasi ya kuingiliwa au kuongezewa majukumu nje ya majukumu yao ya kufundisha
Na  Mwandishi Maalum, New York
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,  Ban  Ki  Moon,  amesema,  utashi wa kisiasa,  matumizi ya  pato  la taifa  na   matumizi ya  fursa mbalimbali unaifanya  Tanzania kuwa moja ya nchi  ya mfano katika  uboreshaji  na upatikanaji wa elimu kwa wote.
Ban Ki Moon  ameyatamka  hayo siku ya  jumapili,  wakati wa hafla ya uzinduzi wa  Ripoti ya Kamisheni ya Kimataifa kuhusu “ Kizazi kinachojifunza: Uwekezaji  katika elimu   kwa dunia inayobadilika”.
Hafla hiyo ilifanyika    Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, na kuhudhuriwa karibu na  Makamishna wote wanaounda tume hiyo akiwamo Rais  Mstaafu wa Tanzania  Mhe. Jakaya  Mrisho Kikwete.
Tume hiyo  ambayo  ipo chini ya  uenyekiti wa   Waziri  Mkuu  Mstaafu wa Uingereza ambaye pia ni Mjuumbe  Maalum wa Katika Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Elimu, inawahusisha pia baadhi ya Marais waliopo madakarani,   Mawaziri  Wakuu  waliopo madarakani  na  waliostaafu,   Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya  Dunia, Mkurugenzi Mtendaji wa UNESCO, Wawekaziji wakubwa akiwamo Bw. Aliko Dangote,   Taasisi za utafiti,   wataalamu wa  masuala  ya fedha, asasi za kijamii  na makundi ya vijana wakiwamo wanafunzi.
“Uzoefu wa nchi kama Tanzania, Vietnam na nchi yangu mwenyewe Korea, unaonyesha  kwamba pale ambapo   pana utashi wa kisiasa, ukijumuishwa na  uwepo wa fursa na  raslimali fedha  kuna  kitu kinachowe kufanyika katika elimu.
Na  kutokana na  uzoefu wa nchi kama Tanzania  na nyinginezo, Mkuu huyo wa Umoja wa  Mataifa   amesema,  Jumuiya ya Kimataifa ni lazima iwe tayari kuzisaidia kwa mitaji  nchi ambazo  zimeamua na kujituma katika kuifanyia mageuzi mifumo yake ya elimu na kujipati matokeo yanayoridhisha.
Jambo kubwa  ambalo limetiliwa mkazo katika ripoti hiyo ni uwekezaji wa raslimali fedha. Kwanza, kwa  kila nchi kukusanya  kutumia mapato yake  ya ndani,  pili misaada kutoka   mashirika ya kimataifa na taasisi za kimataifa,   uwekezaji katika teknolijia ya mawaliano  hususani  internent   ili kutoa fursa kwa wanafunzi kujipatia elimu na maarifa  zaidi nje ya masomo ya darasani.
Akichangia  majadiliano ya uzinduzi wa ripoti hiyo, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete kama mmoja wa  Makamishna na ambaye pia aliongoza majadiliano kuhusu kipengele   cha tatu cha mapendekezo ya  ripoti hiyo kuhusu ujumuishi katika elimu.  Kikwete alikuwa na haya ya kusema.
“Mafanikio ya elimu  lazimia yamfikie kila mmoja    wakiwamo  wale wanaoishi katika mazingira  magugumu  na wanaobaguliwa wakiwamo wasichana”.
Akaongeza  kuwa bahati mbaya leo hii  Afrika Kusini mwa  Jangwa la Sahara  msichana mmoja  kati ya  ishirini wanaoishi katika maeneo  ya umaskini  ndiyo  walio katika   hatua za kumaliza elimu ya msingi.
Rais mstaafu Kikwete  anaeleza kwamba takribani  watoto  milioni 75 ambao wamo katika umri wa kwenda shule wanakabiliwa kila siku na hatari moja ama nyingine. Idadi  hiyo  inajumuisha  watoto  milioni moja wa Syria ambao ni wakimbizi  na ambao hawapati fursa ya kupata elimu.
“Kamisheni hii  inaweka   visheni ya kuwapatia fursa  vizazi vijavyo   huku  mkazo   ukitiliwa pia kwa wakimbizi,watoto wa mitaani,wasichana,watoto walioko katika ajira na makundi mengine ya jamii”. Akasema Rais  mstaafu Kikwete.
Kiwango cha uwekezaji kinachotakiwa kuwekeza ni  kiasi  cha dola   trillion 3 ifikapo mwaka  2030. Aidha  kwa upande wa  nchi ambazo  uchumi wake ni  mdogo zinatakiwa kuwekeza  kutoka asilimia  tatu  ya pato lake hadi  kufikia  asilimia tano ya pato la taifa, wakati zile zenye uchumi wa kati  zitatakiwa kuwekeza  kutoka kiwango cha asilimia  tano ya sasa hadi kufikia asilimia  5.7.
Ili  malengo hayo ya uwekezaji yaweze kufikiwa,    Makamishna kupitia  ripoti yao wanatoa wito kwa Mawaziri wa Fedha kushirikiana na kufanya kati kwa karibu na  Viongozi wao wakuu  wa serikali.
Hata hivyo imeelezwa  pia kupitia ripoti hiyo kwamba  uwekezaji wa raslimali fedha si kigezo  pekee  cha kuwapatia  fursa ya elimu kila mtoto mwenye umri wa kwenda shule.
 Bali  kinachotakiwa pia ni uwekezaji   tangu mtoto anapokuwa tumboni kwa maana ya mzazi kupata  lishe bora na huduma  bora za afya, mtoto anapozaliwa kupata fursa  ya lishe  na makuzi bora, kuwa na fursa ya kupata elimu ya awali ambayo watafiti wanasema ni  jambo la msingi sana katika kumuandaa mtoto.
Vile vile  makamishna wamesisitiza haja na umuhimu wa walimu kuwa sehemu ya mabadiliko ya sekta ya elimu  kwa  wao wenyewe kupatiwa mafunzo ya mara kwa mara, kupewa motisha ya kutekeleza majukumu yao na kuachwa watekeleze  kazi ya ufundishaji pasipo kuingiliwa au kuongezewa majukumu mengine ambayo yapo nje ya kazi yao ya  ualimu.
Makamishna wanatahadharisha  kupitia ripoti hiyo  kwamba kama serikali  hazitafanya haraka kuwekeza  raslimali fesha katika elimu,  watoto katika nchi  zenye  pato dogo la  kiuchumi wataendelea kubaki katika  dimbwi la umaskini  huku wakiwa hawa  ujuzi wala  maarifa  ya aina yoyote ile.
Ripoti inabainisha  zaidi kwamba “ zaidi ya  theruthi mbili ya watoto wenye umri wa kwenda shule katika nchi zenye kipato cha chini hawataweza  kupata maarifa na elimu ya msingi ifikapo  2030 licha ya malengo ambayo  jumuiya ya kiataifa imejiwekea ya kuhakikisha kila mtoto anakwenda  shule”
Inaarifiwa  kupitia  ripoti hiyo kwamba   ni  nusu  tu ya watoto  wote wenye  umri wa kwenda shule ya msingi na zaidi   kidogo ya robo ya wanafunzi wa sekondari katika nchi zenye ukuaji  mdogo wa uchumi  au zile zenye uchumi wa kati ndio wanaopata  fursa ya kujifunza  maarifa/ ujuzi wa awali.
Vile vile  ripoti hiyo imebaini pia kuwa watoto  330 milioni walioko katika shule za msingi na sekondari  wanamaliza elimu yao wakiwa hawajaelimika.
Ripoti hiyo ni  ukamilisho wa kazi ya mwaka mmoja ya uchambuzi uliohusisha zaidi ya  taasisi  30 za utafiti, na  mashauriano yaliyowahusisha zaidi ya  washirika 300 kutoka nchi 105.

No comments: