Advertisements

Friday, September 16, 2016

TCRA YAIFUNGIA RADIO 5 MIEZI 3 PAMOJA NA FAINI, MAGIC FM YAFUNGULIWA KWA MASHARTI

Makamu Mwenyekiti wa kamati ya maudhui Joseph Mapunda akisoma maauzi ya Kamati ya Maudhui 

 Radio 5
Maamuzi ya Kamati ya Maudhui juu ya Radio 5 Kukiuka Kanuni za Utangazaji:
Kituo kilivunja Kanuni za Maudhui kwa Kumkashifu Rais na Serikali na kuchochea na kuhamasisha uvunjifu wa amani, kupambana na Polisi.
Maamuzi:
1. Fine shilingi 5 million
2. Kufungiwa kwa miezi 3
3. Inawekwa chini ya uangalizi kwa mwaka mmoja.

Magic FM

Magic FM yafunguliwa Kamati ya maudhui ya Mamlaka ya mawasiliano Tanzania imekifungulia rasmi kituo cha radio cha Magic Fm cha jijini Dar es salaam

Radio Magic fm ilifungiwa kwa muda usiojulikana na Waziri Nape Nauye Agosti 29, 2016 kwa tuhuma za kutangaza kipindi kinachodaiwa kukiuka sheria za utangazaji
Kwa mujibu wa David Ramadhan aliyekuwepo wakati wa kusoma maamuzi ya kamati ya maudhui ya Mamlaka ya mawasiliano Tanzania, kamati hiyo imeitaka Radio Magic fm kutekeleza yafuatayo..

1)Kutoa onyo kali radio Magic Fm
2)Kuomba radhi kwa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, John Magufuli na wasikilizaji wake, hivyo inatakiwa kuomba radhi kwenye taarifa za habari na tangazo lipewe nafasi kubwa.

No comments: