Trump akizungumza kwenye mkutano wa kampeni huko Arizona.
Trump alitoa hotuba hiyo kwenye jimbo la Arizona wakati akitumia maneno mazito kuliko alivyofanya saa chache kabla alipokuwa nchini Mexico wakati wa kile kilichotajwa kuwa ni mkutano muhimu na Rais wa Mexico Enrique Pena Nieto.
Trump aliendelea kushikilia msimamo wake wa kujenga ukuta kwenye mpaka wa Mexico huku akisema kuwa walizungumzia swala hilo na Rais wa Mexico ingawa Rais huyo alisema wazi kuwa nchi yake haitagharamia ujenzi wa ukuta huo.
Mwenyekiti wa kampeni ya Clinton John Podesta amesema Trump amejikaba mwenyewe kwa kutokuzungumzia suala hilo kwa ukamilifu na rais Pena Nieto.
HABARI KWA HISANI YA VOA-SWAHILI
No comments:
Post a Comment