Advertisements

Thursday, October 13, 2016

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA JOHN MINJA AWASILI MKOANI KILIMANJARO - KUKAGUA ENEO LITAKALOJENGWA KIWANDA KIPYA CHA VIATU

Kamishna Jenerali wa Magereza, CGP- John Casmir Minja(kushoto) akipokea salaamu ya heshima kutoka kwa Afisa wa Jeshi la Magereza Mkoani Kilimanjaro alipowasili Mkoani humo katika ziara ya kikazi ambapo atafanya ukaguzi wa eneo la mradi wa Uwekezaji wa Kiwanda kipya cha Viatu Gereza Karanga, Moshi ambapo mradi huo ni wa ubia baina ya Shirika la Magereza na Mfuko wa Jamii wa PPF, leo Oktoba 13, 2016.
Kamishna Jenerali wa Magereza, CGP- John Casmir Minja akisalimiana na Mkuu wa Magereza Mkoani Kilimanjaro, ACP. Anderson Kamtearo mara baada ya kuwasili Mkoani Kilimanjaro kwa ziara ya kikazi.
Mkuu wa Gereza Kwamugumi, SP. Christopher Mwenda(kushoto) pamoja na Mkuu wa Gereza Korogwe, ACP. Lenard Mushi wakimuongoza Kamishna Jenerali wa Magereza, CGP- John Casmir Minja(kulia) aliposimama kwa muda kukagua Gereza la Wilaya Korogwe wakati akielekea katika ziara yake ya kikazi Mkoani Kilimanjaro, leo Oktoba 13, 2016 (Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

1 comment:

Anonymous said...

Ng'ombe wengi kwa maana ya ngozi za viatu wapo Shinyanga na Mwanza kisha kiwanda cha viatu mwajenga Moshi! Vipi tena?