Advertisements

Saturday, October 15, 2016

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA JOHN MINJA ATEMBELEA ENEO LITAKALOJENGWA KIWANDA KIPYA CHA KUTENGENEZA VIATU, MJINI MOSHI

Kamishna Jenerali wa Magereza - CGP. John Casmir Minja(vazi la kiraia) akiwa ameongozana na Mkuu wa Gereza Karanga, Moshi, ACP. Hassan Mkwiche (kushoto) pamoja na Kaimu Mkuu wa Kiwanda cha Viatu Karanga, ASP. Michael Minja(kulia) alipotembelea Kiwanda hicho ili kuona eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa Kiwanda kipya cha kisasa cha viatu leo Oktoba 14, 2016. Wengine pichani ni Maafisa wa Jeshi la Magereza Mkoani Kilimanjaro.
Kamishna Jenerali wa Magereza - CGP. John Casmir Minja(vazi la suti) akiangalia eneo ambalo limetengwa kwa ajili ya ujenzi wa Kiwanda kipya cha viatu .
Kamishna Jenerali wa Magereza - CGP. John Casmir Minja(vazi la suti) akipata maelezo kutoka kwa Mkuu wa Magereza Mkoa Kilimanjaro, ACP. Anderson Kamtearo(kulia) alipokagua moja ya maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda hicho kipya cha kutengeneza viatu.
Eneo litakalojengwa kiwanda kipya cha kisasa cha kutengeneza bidhaa mbalimbali za ngozi. Kiwanda hicho kitakuwa cha ubia baina ya Shirika la Magereza na Mfuko wa jamii wa PPF.
Kamishna Jenerali wa Magereza - CGP. John Casmir Minja akiangalia kiatu aina ya buti ndefu zinazotengenezwa kiwandani hapo kwa ajili ya Maafisa na Askari wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama kama inavyoonekana katika picha(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

1 comment:

Anonymous said...

Ng'ombe wengi kwa maana ya ngozi za viatu wapo Shinyanga na Mwanza kisha kiwanda cha viatu mwajenga Moshi! Vipi tena?