Advertisements

Wednesday, November 30, 2016

Amplifaya Nov 30 2016...Kauli ya Donald Trump kuhusu wachomao bendera

Rais mteule wa Marekani Donald Trump anaendelea kutawala vyombo vya habari kwa sababu mbalimbali. Moja ni uchaguzi wake, ambao bado wapo wanaoandamana kuupinga, pili ni muendlezo wake katika kutangaza watu anaowateua kuwa sehemu ya serikali yake, na pia, baadhi ya kauli zake anazotoa.
Jana asubuhi, Rais huyo mteule wa 45 wa Marekani alitoa kauli kupitia mtandao wa kijamii juu ya waandamanaji wanaochoma bendera ya Marekani.
Kauli hii imeleta mzozo sana nchini humo, lakini kwa wanaofuatilia kwa makini, kuna mtazamo tofauti juu ya hili.
Mubelwa Bandio, kutoka Washington DC anatueleza kuhusu ujumbe wa Trump, mjadala uliorejea na hata usahihi wa kauli yenyewe na namna inavyoungwa mkono nchini humo

1 comment:

Anonymous said...

Bandio unasauti nzuri,