Advertisements

Thursday, November 17, 2016

KAMPUNI YA HANSPAUL GROUP OF COMPANIES ARUSHA YAIDI KUSHIRIKIANA BEGA KWA BEGA KUSAIDIA MAENDELEO ZAIDI

mmiliki wa kampuni ya hanspaul group of companies Arusha ndugu Hans Paul akiwa anasoma maelezo mafupi ya mradi walioujenga kwa ajili ya wananchi wa kata ya Engutoto pamoja na kata ya Moshono
ndugu Hans Paul katikati akimuonyesha mkuu wa mkoa daraja la zamani ambalo wananchi hao walikuwa wanalitumia
pia viongozi wa vyama mbalimbali walijitokeza katika uzinduzi huo
sehemu ya wafanyakazi wa hanspaul waliouthuria uzinduzi huo
baadhi ya mameneja wa hans paul wakiwa wanafatilia uizinduzi
mkuu wa mkoa na mkurugenzi wa hanspaul group of companies Arusha wakikata utepe kwa ajili ya uhashirikia kuwa daraja limezinduliwa
mkuu wa mkoa wa Arusha akipita juu ya daraja mara baada ya kulizindua rasmi
huu ndio muonekano wa daraja lililo jengwa na kampuni ya Dharam Singh Hanspaul Group 
mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo(kwanza kulia) akizungumza na wadau wa maendeleo Bw. Hans Paul(pili kulia) ambaye aliaidi kutoa mabati ya ujenzi wa zahanati 1000 pamoja na na Bw. Jagjit Aggarwal ambaye aliahidi kutoa mifuko 500 ya cimenti kwa ajili ya ujenzi wa zahanati ya kisasa ya kata ya Engutoto iliopo ndani ya jiji la Arusha

habari picha na Woinde Shizza ,Arusha

Jumla ya zaidi ya shilingi milioni 67.7 zimetolewa na kampuni ya Dharam Singh Hanspaul inaojishulisha na utengenezaji wa bodi za magari ya utalii jijini hapa kwa ajili ya ujenzi wa daraja linalounganisha kata ya Ongutoto pamoja na kata ya Moshono iliopo ndani ya jiji la Arusha .

Akiongea wakati wa kukabidhi daraja hilo mara baada ya kukamilika kwa ujenzi mmiliki wa kampuni hiyo Hans Paul alisema kuwa kampuni yake ipo tayari kushirikiana na kuunga mkono serikali ya awamu ya tano pamoja na serikali ya mkoa wa Arusha katika swala zima la kuleta maendeleo na kusaidia wananchi wa hali ya chini hivyo ndio maana wameamua kuunga mkono serikali kwa kusaidia shughuli mbalimbali za kijiamii ikiwa ni pamoja na kujenga daraja

" sisi kama kampuni ya Dharam singh Hanspaul tunahaidi kushirikiana na serikali ya awamu ya tano katika kila jambo ili kuweza kuwasaidia wananchi wanyonge pamoja na wale wa hali ya chini na tupo tayari kushirikiana na viongozi wa serikali hii bega kwa bega"alisema Hans Paul

Alisema kuwa daraja hilo la Mto kijenge lilianza kujengwa mwezi Juni na kukamilika Agost 2016 lina upana wa Mita 20, uwezo wa kupitisha magari yenye uzito wa Tani tatu(3), urefu kwenda juu ni mita 2.2, uimara wa pekee na linaweza kudumu kwa miaka 50; Ujenzi wake umegharimu kiasi cha shilingi milioni 67 .

Aliongeza kuwa daraja hilo ni ukombozi na msaada kwa wananchi wengi ambao walikua wakipata adha kubwa ya kuvuka haswa wakati wa mvua kutokana na kukosa kivuko cha uhakika na kivuko kilichokuwepo awali kiliashiria hali ya hatari kubwa kwa watoto, wazee, waendesha pikipiki, waenda kwa miguu wote na zaidi hakuna Gari lililokuwa na uwezo wa kupita hapo.

Paul aliongeza kuwa mbali na kujenga daraja hilo pia kampuni yake imejenga madarasa matatu yaliko katika kata ya Engutoto yaliyogarimu kiasi cha shilingi milioni 50 ikiwa ni njia moja wapo ya kusaidia watoto wa kata hiyo kukaa darasani na kusoma kwa raha na amaani zaidi .

“pia mbali na hivyo kampuni hii imeajiri wananchi vijana ambao ni wazawa zaidi ya 500 ambao vijana hawa wanafanya kazi katika kampuni hizi zangu tatu tofauti hii ikiwa ni njia moja wapo ya kuweza kusaidia serikali kutatua tatizo la ajira ambalo linaikamili nchini yetu kwa kipindi hichi na sitaishia apa kwani pia ninampango wa kuendelea kutoa ajira kwa vijana wengine “alisema mmiliki wa kampuni hii ya Dharam Singh Hanspaul

Adha kutokana na kuwa natatizo la kutokuwepo na zahanati katika kata hiyo pia kampuni hiyo iliweza kuhaidi ofisi ya mkuu wa mkoa kuwa itatoa bati 1000 kwa ajili ya zahanati ambayo itajengwa katika kijiji hicho ili wakina mama na watoto waweze kutibiwa kwa uharaka na uhakika zaidi .

1 comment:

Anonymous said...

Sijui ni umaskini ama ni ujinga.