Advertisements

Sunday, November 6, 2016

PROF. NDALICHAKO AFUNGA MKUTANO WA AGA KHAN WA UBORESHANI SEKTA YA ELIMU NCHINI

 Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako akihutubia alipokuwa akifunga mkutano wa wadau wakiwemo wabunge wa kuboresha sekta ya elimu nchini mjini Dodoma jana. Mkutano huo wa siku mbili uliandaliwa na Chuo Kikuu cha Aga Khan.PICHA NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Mkurugenzi wa Chuo Kikuu cha Aga Khan, Profesa JoeLugalla akielezea mambo mbalimbali waliyokubaliana katika mkutano huo jinsi wadau wanavyotakiwa kusaidiana na serikali kuboresha elimu nchini.

 Washiriki wakisikiliza kwa makini wakati Profesa Ndalichako akifunga mkutano huo uliofanyika kwenye Hoteli ya Morena.





 Profesa Ndalichako akiwaeleza washiriki kwamba suala la uboreshaji wa elimu nchini litafanikiwa kwa wadau kushirikiana na serikali.
 Profesa Lugalla akimpongeza Profesa Ndalichako
 Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Kitilya Mkumbo akimpongeza Profesa Ndalichako kwa hotuba yake nzuri.
 Dk. Mkumbo akitoa neno la shukrani kwa Profesa Ndalichako na wadau wengine wa elimu kwa kushiriki katika mkutano huo.
 Meza Kuu ikiongozwa na Profesa Ndalichako wakipiga makofi baada ya kufurahishwa na hotuba ya Dk. Mkumbo
Profesa Ndalichako akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wadau wa elimu walioshiriki katika mkutano huo umuhimu kwa uhai wa elimu nchini.

No comments: