Advertisements

Monday, January 16, 2017

Hatimaye Polisi Geita Wamuachia Edward Lowassa

Waziri Mkuu Mstaafu na Mgombea wa Urais 2015 kupitia CHADEMA, Edward Lowassa leo alikamatwa na jeshi la Polisi wakati akiwa anaenda kwenye kampeni za uchaguzi Kata ya Nkome na baadaye aliachiwa huru ambapo taarifa za polisi zinadai kuwa walimzuia kwa sababu za kiusalama.

Kupitia kituo cha Television cha Azam wameripoti habari ya kukamtwa kwa Lowassa ambapo baadhi wa wananchi wameeleza tukio lilivyotokea.

“Tulikuwa kwenye msafara ya kumpokea Lowassa lakini tulipofika hapa stendi wananchi walitaka kuongea na Lowassa, kabla hata hajashuka kwenye gari askari walituvamia wakasema tuondoke moja kwa moja twende kituoni”– shuhuda.

Mbali na hivyo, Polisi walilazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wananchi wanaoandamana kwenda kituo cha polisi baada ya Lowassa kukamatwa.

Aidha Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita amesema kuwa hawakuwa wamemkamata Edward Lowassa bali walikuwa wakijadiliana naye kuhusu usalama wake na jamii.

GPL

No comments: