Advertisements

Friday, February 24, 2017

MAHIGA ATOA SABABU ZA WATANZANIA KUFUKUZWA MSUMBIJI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Dkt. Augustine Mahiga amesema kuwa Watanzania waliokuwa nchini Msumbiji wamefukuzwa kutokana na kukiuka taratibu na sheria za kuishi nchini humo na akataka suala hilo lisiharibu mahusiano mapana yaliyopo ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Balozi Mahiga alisema Tanzania imekuwa na ushirikiano na Msumbiji kwa muda mrefu hivyo utaratibu walioufuta wa kuwaondoa wahamiaji hao ni wa kiuungwana.

Alisema jana mawaziri wa nchi 14 walianza kuwasili nchini kwa ajili ya kikao cha mawaziri ambacho Tanzania ni mwenyekiti wao, na siyo kwa ajili ya kuzungumzia masuala ya Msumbiji, ila yenyewe ni nchi jirani na watazungumzia masuala ya ulinzi na usalma na ushirikiano wa nchi hizi za SADC.


Alisema watu hao ambao waliingia Msumbiji bila kufuata taratibu, wakiwa huko pia wamevunja sheria za nchi hiyo kwa kujihusisha shughuli bila vibali na kinyume cha taratibu za ajira za nchi hiyo sanjali na kujiingiza katika vitendo vya uhalifu mbaya.

“Watu hawa wanajihusisha na biashara za madawa ya kulevya, silaha na wanapokonya ajira za watu wa nchi hiyo... wahamiaji hao siyo Watanzania pekee, bali na nchi zingine. Lililowagusa zaidi eneo hilo lina madini na linafanana na Mererani na wameanza kufanya biashara hizo kinyume cha Sheria na wameona raia wa Msumbiji hawanufaiki na biashara hiyo,” alieleza.

No comments: