Advertisements

Monday, February 13, 2017

WALIOTAJWA KUHUSIKA NA DAWA ZA KULEVYA KILIMANJARO HAWA HAPA

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro,Kamishna Msaidizi Mwandamizi,Wilbroad Mutafungwa akitaja majina ya watu wanadaiwa kujihusisha na usafirishaji,uuzaji na matumizi ya dawa za kulevya.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro,Wilbroad Mutafungwa akizungumza juu ya msako mkali ulioanza wa kuwakamata wafanyabiashara wa dawa za kulevya katika mkoa wa Kilimanjaro.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro,Wilbroad Mutafungwa akinyunyiza marashi juu ya Mirungi iliyofungwa katika vipande vya magazeti ikiwa ni mbinu mpya inayotumiwa na wasafirishaji wa bidhaa hizo.
Baadhi  ya watuhumiwa wa dawa za kulevya waliokamatwa katika msako uliofanyika kwa muda wa siku nne.
Sehemu ya Misokoto ya Bhangi iliyokamatwa wakati wa opereshni hiyo .

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

JESHI la Polisi mkoa wa Kilimanjaro limetaja majina ya watu 47 wanaotuhumiwa kuhusika katika  kusafirisha,kuuza na kutumia dawa za kulevya huku likifanikiwa kukamata misokoto 269 na miche 13 ya Bhangi,pamoja na kilogramu 32.9 za mirungi pia ikikamatwa.

Kukamatwa kwa watuhumiwa hao pamoja na dawa hizo za kulevya kunatokana na msako mkali uliofanywa na kikosi maalumu cha jeshi hilo kwa muda wa siku nne katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Kilimanjaro .

Akitangaza majina hayo ofisini kwake ,Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro ,Kamishna Mwanadamizi Msaidizi wa Polisi,Wibroad Mutafungwa alisema watuhumiwa hao tayari wamekamatwa na wako katika hatua mbalimbali za kiupelelezi na taratibu zikikamilika watafikishwa mahakamani.

Miongoni mwa watuhumiwa 47 wamo watoto wawili  waumri wa miaka 17 ambao ni Wilfred Mnubi mkazi wa Bomang’ombe wilaya ya Hai na Ruben Bakari mkazi wa Njoro katika manispaa ya Moshi.

Kati ya watuhumiwa hao wanawake ni 15 na wanaume ni 32 akiwemo mzee mwenye umri wa miaka 60,Christina Ferdinand.

“Vita hii tumeianza tangu mwaka juzi,tunajua vita hii ni kubwa bahati nzuri ni kwamba njia wanazotumia wafanyabiashara wa dawa za kulevya husani mirungi na bhangi ,tayari jeshi la polisi limezibaini,maeneo ambayo dawa za kulevya zimekithiri Jeshi la polisi limekwisha baini ,operesheni hii ambayo tumeianza ni endelevu na tutaendelea kuwakamata watu hawa kwa kutumia mbinu zote tulizonazo.”alisema Mutafungwa

Waliotajwa na kushikiliwa na jeshi la Polisi ni pamoja na:
(1)         Juma Kabwele(25).
(2)         Mohaed Kabwele (29) .
(3)         Shabani Mponda(39).
(4)         Khadija Mushiri(27).
(5)         Veronika Chuwa (39).
(6)         Mwanahamis Hussein.
(7)         Yusuph Issa(42).
(8)         Salim Massawe(48).
(9)          Hadija Mohamed(50).
(10)       Shenein Abilah(41).
(11)        Husna Mgonja(24).
(12)       Najima Desouza (46) .
(13)       Ruben Bakari (17) .
(14)       Paul Kisoka (26).
(15)       Raphael Mbuya (40).
(16)       Wilfred Mnubi(17).
(17)       Athuman Swaehe (35).
(18)       Joseph Hamis(20).
(19)       Zuber Temu(27).
(20)      Robert Kitika (18) .
(21)       Mohamed Juma (25).
(22)       Ahmad Shaban (57).
(23)      Donas Masashua(22).
(24)      Japhet Tungai (46).
(25)      Asima Mndeme (24).
(26)      Muutaz Zalia ,
(27)      Noah Singano (29).
(28)      Ramadhan Masale (40) .
(29)      Kirambati Swai(45).
(30)      Said Mrii.
(31)      Erick Henry (20).
(32)      Seif Ally(20).
(33)      Ramadhan Hassan (36).
(34)      Victor John(22).
(35)      Upendo Endkia (42).
(36)      Asia Ally(39).
(37)      Catherine Linusi (36) .
(38)      Mariam Hemed (44) .
(39)      Mwajuma Msuya (48).
(40)      Juma Yusuph (22) .
(41)      Hussein Anyokisye (17).
(42)      Musa Msangi (30).
(43)      Ramadhani Hassan (36).
(44)      Wilfred Munubi(17)
(45)       Ruben Bakar.(17)
(46)       Christina Ferdinand.(60)
(47)       Samweli Kingai(42).

No comments: