Advertisements

Thursday, March 23, 2017

NAPE AOONYESHWA BASTOLA ALIPOKUA AKIONGEA NA WAANDISHI WA HABARI

4 comments:

Anonymous said...

Tuachane na masuala ya bastola lakini utaona jinsi gani Nape alivyokuwa mtu wa mihemko isiyokuwa na maana. Katika akili ya haraka haraka kama muajiri wako kakuachisha kazi lazima atakuwa ni mtu wa kwanza unatakiwa kuwasiliana naye na kupata maelezo kamili juu ya kosa lako la kukatishwa ajira. Cha kushangaza na ajabu Nape ana kiri kwenda kufanya mkutano na waandishi wa habari kwanza kabla bila ya kupata maelezo mubashara kutoka kwa bosi wake ya nini kilichompelekea kumkatisha ajira. Anaonekana kuwaambia watu wasipanik lakini ni yeye Nape mwenyewe binafsi kuonekana kupanic chakari. Binafsi namkubali Nape lakini anatakiwa kukuwa kiakili na ku behave like professional baada ya kuropokwa hovyo.

Anonymous said...

VERY SAD TO SEE YOU GO JUST LIKE THAT NAPE. KUNA HATARI RAIS WETU ATAIGAWA NCHI YETU. NINA UHAKIKA ITAKUWA NI VIGUMU TENA KWA YEYE KUPATA KURA NYINGI KUTOKA MIKOA YA KUSINI NA KANDA YA NYANDA ZA JUU ZA KUSINI KATIKA UCHAGUZI UJAO. HAWEZI KUWATIMUA, KUTOWATENDEA HAKI NA KUWADHALILISHA WANASIASA WA KUSINI, AMBAO WAPO WENGI NA MAJINA TUNAYO. HATA KAMA ATAIJAZA SERIKALI YOTE NA WATU KUTOKA KANDA YA ZIWA, CCM HAINA NGUVU BILA MIKOA YA KUSINI. HAYATI MWALIMU NYERERE ALILITAMBUA HILO. KUSINI NA NYANDA ZA JUU ZA KUSINI ZIMEKUWA DAIMA NGOME YA CCM. PIA RAIS AKUMBUKE KUWA, KAMA ISINGEKUWA JITIHADA ZA MWANASIASA WA KUSINI RAIS MSTAAFU MKAPA KUMPIGIA DEBE ASINGEPATA KUWA MTEULE WA CCM, NA HIVYO ASINGEKUWA RAIS. NAPE NNAUYE NDIYE ALIYEFANYA KAZI KWA BIDII SANA KUWAONGOZA VIJANA WAMPIGIE DEBE RAIS NA KUKAMPENI KWA AJIRI YAKE, NA HIVYO KUIBUKA MSHINDI DHIDI YA LOWASA. TAFADHALI MHESHIMIWA RAIS, JITAHIDI KUIWEKA TANZANIA YETU NCHI YENYE MSHIKAMANO, KWANI NI WATANZANIA NDIYO TULIKUCHAGUA UWE RAIS WETU, HIVYO USIWACHUKIZE SANA WAPIGA KURA WENGI AMBAO UTAWAHITAJI SIKU ZA USONI.

Anonymous said...

Anonymous @ 7:10 PM acha kuleta ushabiki, unless wewe umetumwa kuandika maoni hayo. Nape ni mwanasiasa kama Rais. Nape hakufungwa mdomo na hakuna sheria inayosema kuwa haruhusiwi kuzungumza na Wanahabari. Ni jukumu la Rais aliyemteua kumwambia kwa nini amemwachisha Uwaziri. Rais aliyemteua Nape aliwajibika (PROFESSIONALLY) kumuita, kumuandikia au kumpigia simu Nape. Kutomfanyia hivyo ilikuwa na lengo la kumdhalilisha Mbunge ambaye amechaguliwa na Wananchi wa Mtama. Rais alichaguliwa na sisi Wananchi wa Tanzania, Nape pia alichaguliwa na Wananchi wa jimbo lake, hivyo wote wanazo kazi muhimu za kuwafanyia Wananchi. Uwaziri siyo ajira, bali ni majukumu tuu unayopewa na mwanasiasa mwenzio(Rais). Wananchi wa jimbo la mtama ndiyo wamemwajiri ndugu Nape, kazi ambayo hakuna kiongozi mwingine anaweza kumfukuza, including Rais wa Jamhuri. Hivyo basi, hii kebehi yako ya kusema "Nape anatakiwa kukuwa kiakili na ku behave like professional" doesn't make sense at all. Apparently, you are the one behaving unprofessionally, kwa sababu unaunga mkono kitendo ambacho siyo cha kiungwana kumlaumu Nape kwa kufanya mazungumzo na Wanahabari. Hata wewe unaweza na unayo haki ya kawaita Wanahabari na kuzungumza chochote cha moyoni mwako. Tanzania is a free society (I suppose), we are not in a dictatorship. It is people with mindset like yours who are drifting Tanzanians backward. Nakuomba uamke mdau, hii ni karne ya Ishirini na Moja tusijirudishe nyuma kifikra kwenda enzi za Stone Age.

Anonymous said...

Mheshimiwa mmiliki wa blogu hii tafadhali tunakuomba uache censorship, kwani unakiuka freedom of expression. Hii ni Marekani, ni vyema uruhusu free speech, no matter how unpalatable it is. On several occasions wadau wanatoa maoni na comments zao, ambazo kwa standards za hapa Marekani ni permissible lakini wewe unazifinya. You are breaking the law. Tunazo data za kuthibitisha hili. Tafadhali waruhusu wadau wayatoe ya moyoni unapochapisha hoja zinazowakera. Usibague au kuwa selective. The First Amendment ni muhimu sana na lazima iheshimiwe, kwa sababu blogu hii imeandikishwa hapa Marekani na siyo bongo. Serikali ya Tanzania haiwezi kuizuia blogu yako au kuku-censure maana sheria zitakulinda. Wapo Wanasheria (tunawajua) mahiri hapa Marekani watakutetea kama utakuwa censured na Serikali ya JPM. Wadau tunaipenda sana blogu yako, na tunakushukuru sana but you need to rectify upokeaji wa hoja zote za wadau. Asante sana mpwa.