Advertisements

Friday, May 26, 2017

Amuua mke wake kwa kumpiga risasi, naye ajiua

By Jesse Mikofu, Mwananchi jmikofu@mwananchi.co.tz

Mwanza. Mkazi wa Mahina, jijini Mwanza, aliyefahamika kwa jina moja la Max, anadaiwa kumuua mke wake, Teddy Malulu kwa kumpiga risasi usiku wa kuamkia leo.

Baada ya kufanya mauaji hayo, Max naye anadaiwa kujiua kwa kujipiga risasi.

Mpaka sasa chanzo cha mauaji hayo hakijajulikana.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza Ahmed Msangi amethibitisha tukio hilo na kusema kuwa mwanamke anayedaiwa kuuawa na mume wake ni Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Wavuvi Tanzania (Tafu) .

Kamanda Msangi amesema uchunguzi wa tukio hilo bado unaendelea.

No comments: