Advertisements

Friday, May 26, 2017

BALOZI SEIF AKUTANA NA UJUMBE WA BENKI YA DUNIA NA WASHIRIKA WAKE

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na Mwakilishi wa Benki ya Dunia Bwana Moderes Abdula aliyeuongoza Ujumbe wa Washirika wa Maendeleo ulikuwepo Zanzibar kwa siku Nne kukagua miradi ya Tasaf Awamu ya Tatu. Kati kati yao ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Tanzania Bwana Ladislas Mwamanga.
Balozi Seif akizungumza na Ujumbe wa Benki ya Dunia ulioambatana na washirika wa Maendeleo hapo Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar uliofika kukagua miradi ya Tasaf.

Balozi Seif kati kati waliokaa vitini akiwa katika picha ya pamoja na Ujumbe wa Viongozi wa Benki ya Dunia na washirika wake wa maendeleo mara baada ya kumaliza mazungumzo yao.  Kushoto ya Balozi Seif ni Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mh. Mihayo Juma Nhunga, Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Nd. Joseph Abdulla Meza na Bibi Azzah Ammin kutoka Shirika la Idadi ya Watu Duniani (UNFPA).  Kushoto ya Balozi Seif ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Jamii Tanzania (TASAF) Nd. Ladislas Mwamanga, Mwakilishi wa Benki ya Dunia Bwana Moderes Abdula na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Nd. Ahmad Kassim Haji.
Balozi Seif akiagana na Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Jamii Tanzania (TASAF) Nd. Ladislas Mwamanga wakishuhudiwa na Mwakilishi wa Benki ya Dunia Bwana Moderes Abdula.


Picha na – OMPR – ZNZ.
Benki ya Dunia kupitia washirika wake wa Maendeleo imeamini ya kuridhika na hatua kubwa iliyochukuliwa na Jamii ya Wananchi wa Visiwa vya Zanzibar katika kusimamia miradi yao kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Tanzania{TASAF} Awamu ya Tatu katika kujiondolea Umaskini.


Viongozi wa Ujumbe wa Washirika hao wa Maendeleo ulitoa kauli hiyo wakati ukitoa tathmini ndogo kwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar baada ya kumaliza ziara yake ya kukagua miradi ya Jamii inayotekelezwa kupitia Tasaf Tatu katika maeneo mbali mbali ya Mjini na Vijijini Unguja na Pemba.

Kiongozi wa Ujumbe huo kutoka Benki ya Dunia Bwana Moderes Abdulah alimueleza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwamba ziara ya Ujumbe wake imeshuhudia maendeleo makubwa yaliyopatikana katika Jamii kutokana na kundi kubwa la Wananchi lilivyoamua kutekeleza kwa ufanisi mkubwa miradi yao waliyoianzisha. 

Bwana Moderes alisema Zanzibar imeonyesha mfano bora katika uendelezaji wa miradi ya Maendeleo kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Tanzania {TASAF} awamu ya Tatu kiasi kwamba Uongozi wa Benki ya Dunia kupitia Washirika wake imefurahia hatua hiyo ya mafanikio.

Alifahamisha kwamba Benki ya Dunia kupitia washirika wake imeamua kuunga mkono miradi ya Maendeleo kwa Wananchi Maskini katyika Nchi zinazoendelea ikilenga kuona ufanisi wa kudumu unapatikana katika kustawisha maisha yao ya kila siku.

Wakitoa ufafanuzi zaidi wa ziara hiyo ya kukagua Miradi ya Tasaf Visiwani Zanzibar Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Tanzania Bwana Ladislas Mwamanga na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa ya Kuhudumia Watoto { UNICEF} Bwana Paul Quarles walisema upo ushahidi wa fedha zainazotolewa na Tasaf kutumika katika utaratibu Maalum uliowekwa.





Walisema ujenzi wa nyumba za kudumu, upatikanaji wa sare za skuli, uanzishwaji wa Vitalu vya miti ya kudumu, ujenzi wa majengo ya Skuli na Madrasa kwa kaya Maskini ni mfanbo wa matumizi hayo sahihi ya fedha hizo.

Wameipongeza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Watendaji wa Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibarpamoja na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kwa usimamizi wake mzuri kwenye miradi ya Mfuko huo wa Tasaf.

Akitoa shukrani zake Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema Benki ya Dunia kupitia Wadhirika wake wa Maendeleo haikupoteza Fedha iliyotoa katika kuanzishwa kwa Mradi huo.

Balozi Seif alisema Mfuko wa Tasaf tokea kuanzishwa kwake katika awamu zote mbili zilizopita imeibua miradi mingi ya Jamii katika maeneo mbali mbali Unguja na Pemba na kuweza kusaidia ajira na kupunguza Umaskini.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kupitia Ujumbe huo ameiomba Benki ya Dunia kuendelea kuiunga mkono Zanzibar na Tanzania kwa ujumla katika harakati za kupambana na ukali wa maisha na kustawisha Jamii.

Ujumbe huo wa Viongozi wa Benki ya Dunia ulioambatana na Washirika wake wa Maendeleo yakiwemo Mashirika ya Umoja wa Mataifa Kuhudumia Watoto { UNICEF} na lile la Idadi ya Watu {UNFPA}na Viongozi wa Tasaf Bara na Zanzibar walikuwepo Zanzibar kwa ziara ya siku Nne kukagua Miradi ya Tasaf.

Othman Khamis Ame

Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
26/5/2017.

No comments: