Advertisements

Wednesday, May 31, 2017

MKUU WA MKOA WA ARUSHA,MRISHO GAMBO AMPONGEZA MFUGAJI KWA KUWEKEZA KWENYE HOTELI

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kirutheri Tanzania(KKKT)Dayosisi ya Kaskazini Kati,Solomon Masangwa akizumza katika sherehe ya uzinduzi wa hoteli ya Eseriani Kata ya Levolosi jijini Arusha na kumpongeza mmiliki kwa kufuga kisasa na kuwekeza kwa kutoa ajira na kuongeza huduma bora kwa wageni wanaofika Arusha
Mkuu wa wilaya mstaafu,,Peter Toima akitoa salamu zake kwa wananchi walihudhuria.

Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo akizungumza katika sherehe hiyo,kulia ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)mkoa wa Arusha,Michael Lekule Laizer.
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kirutheri Tanzania(KKKT)Dayosisi ya Kaskazini Kati,Solomon Masangwa akikata utepe kuashiria uzinduzi wa hoteli hiyo wanaoshuhudia kushoto ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Arusha,Michael Lekule Laizer na Mkuu wa mkoa,Mrisho Gambo.
Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo akizindua hoteli ya Eserian ,kulia ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)mkoa wa Arusha,Michael Lekule Laizer.
Mmiliki wa hoteli ya Eserian,Issaya Yassi(kulia)akimweleza Mkuu wa mkoa,Mrisho Gamb(wa pili kushoto),Askofu Masangwa(kushoto) na Mwenyekiti CCM mkoa wa Arusha,Michael Lekule Laizer namna alivyotumia mifugo kuwekeza kwenye nyumba ya wageni.
Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo akiangalia mandhari ya hoteli ya Eserian akiwa na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)mkoa wa Arusha,Michael Lekule Laizer.
Mfanyabiashara maarufu wa jijini Arusha,Philemon Mollel maarufu kwa jina la Monaban (kushoto) akikabidhiwa tuzo maalumu na Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo iliyotolewa na shirika la kidini World Mission International kwa kutambua mchango kwa jamii.

No comments: