Advertisements

Wednesday, June 28, 2017

KOCHA JOSE MOURINHO AENDA URENO KUMZIKA BABA YAKE



Kocha wa Manchester United Jose Mourinho amewasili Ureno kuhudhuria mazishi ya baba yake mzazi yanayofanyika hii leo.



Mourinho ameonekana akihudhuria misa iliyofanyika Setubal akiwa na marafiki na familia yake hapo jana baada ya kutokea kifo hicho.



Marehemu Jose Manuel Mourinho Felix, ambaye alikuwa akiugua kwa miezi kadhaa, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 79 siku ya jumapili huko Setubal.
                   Kocha Jose Mourinho akipewa pole kufuatia kifo cha baba yake mzazi

No comments: