Advertisements

Thursday, June 1, 2017

MAKUMI WAFUNGULIWA KWENYE MKUTANO WA OYES 2017 JIJINI MWANZA.

Makumi ya wakazi wa Jiji la Mwanza na viunga vyake waliohudhuria kwenye mkutano wa Injili wa OYES 2017 (Open Your Eyes and See) jana wamefunguliwa na kumpokea Kristo.

Kabla ya kuanza mkutano huo, Mchungaji Garry White (kushoto) kutoka Marekani alitoa semina kwa akina mama, vijana na wanandoa ambapo tamati ya mkutano huo unaofanyika viunga vya Kanisa la EAGT Lumala Mpya, nyumba ya Soko Kuu la Sabasaba Jijini Mwanza ni jumapili June 04,2017.

Mchungaji Kiongozi wa Kanisa hilo, Dkt.Daniel Kulola, amewasihi watu wote kuhakikisha wanahudhuria mkutano huo uliojaa mahubiri na mafundisho ya neno la Mungu yakilenga kumfungua kila mmoja ili kuuona Ukuu na Utukufu wa Mungu.
#BMGHabari
Mchungaji Garry White kutoka Marekani akihudumu kwenye mkutano wa OYES 2017

Mchungaji Garry White kutoka Marekani akihudumu kwenye mkutano wa OYES 2017
Mchungaji Dkt.Daniel Moses Kulola, akihudumu kwenye mkutano wa OYES 2017
Ibada ya kuabudu ikiendelea
Wakazi wa Jiji la Mwanza wakifuatilia mafundisho kwenye mkutano wa OYES 2017 Kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza
Mkutano huu ulianza jumamosi Mei 27 na utafikia tamati jumapili June 04,2017. Muda ni kuanzia saa tisa na nusu mchana isipokuwa jumapili ambapo ibada zitaanza asubuhi.

No comments: