Advertisements

Sunday, June 11, 2017

NAIBU WAZIRI MH. LUHAGA MPINA AFANYA UKAGUZI KATIKA MAENEO YA BOKO BUNJU TEGETA NA KEKO MWANGA.

 Mtaro wa maji Machafu uliokuwa ukilalamikiwa na wakazi wa keko mwanga katika mtaa wa Mafuta.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais- Mazingira na Muungano Mh. Luhaga Mpina (Katikati)  akimsikiliza katibu wake Bw. Daniel Sagata (kulia) alipokuwa akizungumza kuhusu sehemu ya ukuta wa kiwanda cha red sea uliobomolewa kupisha maji ya mvua, wakati wa ukaguzi wa utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa katika ziara yake alipotembelea katika eneo la keko mwanga mtaa wa Mafuta kushoto ni Bw. Salea Haffif mwakilishi wa kiwanda cha Red Sea.
 Kushoto Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais- Mazingira na Muungano Mh. Luhaga Mpina akimsikiliza katibu wake Bw. Daniel Sagata  kulia alipokuwa akimuonyesha tuta lililojengwa na kiwanda cha saruji cha Wazo cha Tegeta Jijini Dar es Salaam, Tuta ambalo  lilijengwa baada ya kujengwa mtaro wa kupitisha maji ya mvua yaliyokuwa yakisababisha kero ya mafuriko kwa wakazi wa maeneo jirani yaliyotaka na makorongo yaliyochimbwa na kiwanda hicho kwa lengo la kutafuta maligafi za kutengeneza saruji, kero hiyo inasemekana kupungua baada ya Naibu Waziri Mpina kuwahai kufanya ziara kiwandani hapo na kutoa maagizo.
 Sehemu ndogo ya korongo inayomwaga maji ya mvua na kuingia katika mfereji uliojengwa na kiwanda cha wazo.
Kushoto Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina Kiongea na vijana katika eneo la Bunju A Usalama, kuhusu Karavati (halipo pichani) ambalo lilikuwa ni moja ya kero ya kuchangia mafuriko katika eneo hilo hasa katika vipindi vya mvua kutokana na uchafu wa mazingira uliopelekea karavati hilo kuziba. Naibu Waziri Mpina ametembelea eneo hilo leo ikiwa ni sehemu ya ufuatiliaji wa utekelezaji wa  magizo aliyotoa kwa sekta husika wakati wa ziara yake aliyowahi kuifanya katikamaeneo hayo.

No comments: