Advertisements

Sunday, July 9, 2017

WATEMI WA KISUKUMA, VIONGOZI WA TAS WAIBUKIA KITUO CHA WATOTO WENYE UALBINO SHINYANGA


Watemi wa Kisukuma Kanda ya Ziwa Victoria na viongozi wa Chama Cha Watu Wenye Ualbino nchini Tanzania( Tanzania Albinism Society -TAS) wamefanya usafi wa mazingira kisha kula chakula cha pamoja na watoto wenye ualbino wanaolelewa katika kituo cha Buhangija katika manispaa ya Shinyanga.

Watemi hao wakiongozwa na Katibu Watemi wa Kisukuma Kanda ya Ziwa, Mtemi Charles Balele Itale wa Bujashi wilaya ya Magu mkoa wa Mwanza walitembelea kituo hicho Jumamosi Julai 8, 2017. 
Mwenyekiti wa Chama Cha Watu Wenye Ualbino nchini Tanzania -TAS taifa, Nemes Temba alisema chama hicho kimekuwa na ushirikiano mkubwa na machifu wa kanda ya ziwa hicho kuamua kushiriki nao katika kufanya usafi wa mazingira katika kituo cha Buhangija. 
“Malengo ya kuja hapa kwanza ni kuunga mkono serikali ya awamu ya tano kuhusu masuala ya usafi,pili ni kuwapa ujumbe watoto hawa kuwa wawe na utamaduni wa kufanya usafi hata wanaporudi kwenye familia zao,tatu tumekuja kula chakula cha pamoja na watoto hawa ili kuonesha kuwa tuko pamoja nao”,alieleza Temba. 
Temba alitumia fursa hiyo kuiomba serikali kuchunguza utitiri wa mashirika yaliyoanzishwa nchini ambapo sasa yapo zaidi ya 10 na kufuatilia vituo mbalimbali vilivyoanzishwa kwa lengo la kuwahudumia watu wenye ualbino hususani watoto kwani sasa vipo takribani 20 lakini wahusika wa vituo hivyo hawasaidii walengwa.
Temba alisema mashirika mengi yamekuwa yakijikita katika kupiga vita mauaji ya watu wenye ualbino huku yakisahau kuwa watu wenye ualbino wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo ukosefu wa elimu na saratani ya ngozi ambayo imekuwa ikiua watu wengi wenye ualbino. 
 Katibu Watemi wa Kisukuma Kanda ya Ziwa, Mtemi Charles Balele Itale wa Bujashi wilaya ya Magu mkoa wa Mwanza alimpongeza mwenyekiti wa Chama cha Watu wenye Ualbino kuwakutanisha pamoja katika kituo hicho. 
“Juhudi hizi zinaonesha jinsi tunavyowatambua,tunavyowapenda na tunavyowajali watu wenye ualbino,kwa hiyo katika nafasi zetu za nyadhifa mbalimbali tunajitahidi kuelimisha na kuwezesha jamii iwatambue,iwajali,iwapende na kuwapokea katika jamii na watoto warudi kwenye familia zao na kuishi kama watoto wengine”,alieleza Mtemi Balele. 
“Nimefurahishwa na taarifa ya uongozi wa kituo hiki kuwa sasa watoto wameanza kwenda likizo kuwaona wazazi wao,hili ni jambo jema sana,Sisi machifu tuna jukumu letu ni kuielimisha jamii iwapokee,iwakubali,isiwanyanyase,isiwanyanyapae hivyo sisi kwa kushirikiana na TAS tutashirikiana katika kutafikia hayo malengo”,aliongeza Mtemi Balele. 
Awali akizungumza katika kituo hicho,Mwalimu Mlezi wa Shule ya Msingi Buhangija, Frola Kakutebe alisema kati ya watoto wenye ualbino 140,waliopo katika kituo hicho,72 wameenda likizo na 68 wamebakia kituoni baada ya shule kufungwa kinyume na miaka ya nyuma ambapo watoto hao walikuwa hawaendi likizo kuonana na ndugu zao. 
Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Selemani Kipanya aliiambia Malunde1 blog kuwa,sasa Kituo hicho kimepoteza sifa ya kuitwa kituo bali ni shule kwani tofauti na siku za nyuma hivi sasa watoto wanaoishi hapo wote wanasoma shule na wanaishi katika mabweni yaliyopo katika shule hiyo. 
Katibu Mtendaji wa Chama Cha Watu Wenye Ualbino nchini Tanzania -TAS taifa,Mussa Mussa akizungumza katika kituo/Shule ya Msingi Buhangija katika manispaa ya Shinyanga.Kulia ni Katibu wa Umoja wa Watemi wa Kisukuma kanda ya Ziwa, ambaye ni chifu/mtemi wa Bujashi wilaya ya Magu mkoa wa Mwanza Charles Dotto Balele.Kushoto ni Mwalimu Mlezi wa Shule ya Msingi Buhangija, Frola Kakutebe-Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog
Katibu wa Umoja wa Watemi wa Kisukuma kanda ya Ziwa, ambaye ni chifu/mtemi wa Bujashi wilaya ya Magu mkoa wa Mwanza Charles Dotto Balele Itale akizungumza katika kituo cha Buhangija.Kulia ni Mwenyekiti wa Chama Cha Watu Wenye Ualbino nchini Tanzania -TAS taifa, Nemes Temba 
Mtemi Balele akizungumza katika kituo cha kulelea watoto wenye ualbino cha Buhangija.
Kushono Mwenyekiti wa Chama Cha Watu Wenye Ualbino nchini Tanzania -TAS taifa, Nemes Temba akifuatiwa na Mtemi Nyamilonda III Mikomangwa Aron wa Mwanza 'Ng'wanza (katikati),kulia ni Mtemi Wenceslaus Seni wa Kanadi mkoani Simiyu wakiwa eneo la tukio. 
Kushoto ni Mtemi Wenceslaus Seni wa Kanadi mkoani Simiyu,akifuatiwa na Mtemi Charles Gagambaseni Dogani wa Seke - Kishapu mkoani Shinyanga,kulia ni Mtemi Charles Lubasha Kimwaga Kaswende wa Luhumbo mkoani Shinyanga.
Mwenyekiti wa Chama Cha Watu Wenye Ualbino nchini Tanzania -TAS taifa, Nemes Temba akizungumza katika kituo cha Buhangija ambapo aliiomba serikali kuona umuhimu wa kuwapa nguvu viongozi wa kimila kama zamani kwani wanazungukwa na watu wengi hivyo kuwa na nafasi kubwa ya kuleta mabadiliko katika jamii.
Watoto,walimu na maafisa kutoka TAS wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea
Mwenyekiti wa Chama Cha Watu Wenye Ualbino nchini Tanzania -TAS taifa, Nemes Temba akizungumza katika kituo cha Buhangija.
Mwenyekiti wa Chama Cha Watu Wenye Ualbino nchini Tanzania -TAS taifa, Nemes Temba akizungumza.
Mwenyekiti wa Chama Cha Watu Wenye Ualbino nchini Tanzania -TAS taifa, Nemes Temba akisisitiza jambo.
Watoto na maafisa kutoka TAS wakiwa eneo la tukio
Katibu wa Umoja wa Watemi wa Kisukuma kanda ya Ziwa, ambaye ni chifu/mtemi wa Bujashi wilaya ya Magu mkoa wa Mwanza Charles Dotto Balele Itale akila chakula na watoto wanaolelewa katika kituo cha Buhangija katika manispaa ya Shinyanga.
Mtemi Wenceslaus Seni wa Kanadi mkoani Simiyu akila chakula na watoto wa wanaolelewa katika kituo cha Buhangija,ambapo wapo wenye ualbino,wasiosikia na wasioona.
Mwenyekiti wa Chama Cha Watu Wenye Ualbino nchini Tanzania -TAS taifa, Nemes Temba,Mtemi Wenceslaus Seni wa Kanadi mkoani Simiyu na Mtemi Charles Gagambaseni Dogani wa Seke - Kishapu mkoani Shinyanga wakila chakula na watoto kituo cha Buhangija.
Mtemi Charles Gagambaseni Dogani wa Seke - Kishapu mkoani Shinyanga akila chakula na watoto.
Watemi na Viongozi wa Chama Cha Watu Wenye Ualbino nchini Tanzania -TAS wakiendelea kula chakula na watoto katika kituo cha Buhangija.
Mtemi Charles Lubasha Kimwaga Kaswende wa Luhumbo mkoani Shinyanga akila chakula na watoto.
Mtemi Nyamilonda III Mikomangwa Aron wa Mwanza 'Ng'wanza akila chakula na watoto.
Afisa Mahusiano na Habari kutoka chama cha watu wenye ualbino Tanzania (TAS)Josephat Torner akila chakula na watoto.
Kushoto ni Katibu wa Umoja wa Watemi wa Kisukuma kanda ya Ziwa,Charles Dotto Balele Itale ambaye ni Mtemi wa Bujashi wilaya ya Magu mkoa wa Mwanza akifuatiwa na Afisa Mahusiano na Habari kutoka chama cha watu wenye ualbino Tanzania (TAS) Josephat Torne (katikati) na Afisa Programu kutoka Chama cha watu wenye ualbino Tanzania Severin Edward wakifanya usafi katika kituo cha kulelea watoto wenye ualbino cha Buhangija manispaa ya Shinyanga.
Mtemi Wenceslaus Seni wa Kanadi mkoani Simiyu akifanya usafi karibu na choo wa watoto katika kituo cha Buhangija.
Mtemi Nyamilonda III Mikomangwa Aron wa Mwanza 'Ng'wanza akiweka uchafu kwenye ndoo. 
Kulia ni Afisa Programu kutoka Chama cha watu wenye ualbino Tanzania Severin Edward na Mwalimu Mlezi wa Shule ya Msingi Buhangija, Frola Kakutebe wakifanya usafi katika kituo cha Buhangija.

No comments: