Advertisements

Friday, August 18, 2017

Mwanamke aliyejeruhiwa na mke wa Rais Mugabe apigiwa magoti

Familia ya mwanamke aliyedaiwa kushambuliwa na Bi Grace Mugabe imedaiwa kufuatwa na kuombwa na mtu asiyejulikana kukubali fedha kama fidia ya kutupilia mbali kesi hiyo, wakili wake amesema.
Familia haitaki kufanya hivyo, Gerrie Nel alisema.”Walisema tuzungumze na tuwache kesi hii, lakini hakuna kiwango cha fedha kilichotajwa,” aliongezea.
Wakati huohuo katika mahojiano marefu ya simu na bi Gabriella Engels ambaye amemtuhumu bi Grace Mugabe kwa kumpiga, Mwandishi wa BBC Pumza Fihlani alitulia na kuonekana kuwa mtu aliyekuwa na wasiwasi mwingi mara kwa mara.
Akielezea tukio hilo bi Engels mwenye umri wa miaka 20 alisema kuwa yeye na watu wengine wanne, wawili wakiwa wana wa kiume wa rais Mugabe na bi Grace Mugabe walikuwa wakinywa vinywaji siku ya Jumapili usiku katika chumba kimoja cha hoteli mjini Sandton, makaazi ya kifahari yaliopo Johannesburg.
Baadaye alienda katika chumba chengine na bi Mugabe akamfuata akiwatafuta wanawe.
Bi Mugabe alikuwa ameshikilia waya wa umeme mkononi mwake….alinizuia na kuanza kunipiga .
Nilijiangusha chini na kuanza kubingirika ili kukwepa kichapo hicho, na ni hapo aliponipiga na waya hiyo. Na nakumbuka nikiwa katika sakafu huku nikiwa nimejaa damu usoni na shingoni, bi Engels alidai.
Nilikuwa nikifikiria nitoke katika chumba hicho kabla ya mwanamke huyu kuniuwa.
Watu waliokuwa katika chumba hicho ni walinzi wake na walikuwa wamesimama nyuma yake huku akitupiga.
ulimsihi kuwacha kufanya hivyo ,lakini hakutaka kusikia aliendelea kutupiga…alitupiga akiwa na chuki nyingi .
Hadi leo marafiki zangu sielewi kwa nini mwanamke huyu alitushambulia vile bila ya sababu yoyote, Engels aliongezea.
kabla nitambue alikuwa bi Mugabe, nilijua nilifaa kumshtaki kwa kunishambulia kwa kuwa nilijeruhiwa vibaya
Sikujua yeye ni nani. na nilipojua yeye ni nani, sikutaka kumshtaki .. lakini mamangu akanisukuma kuwasilisha mashtaka hayo mahakamani, kwa sababu aliniambia: Kile mwanamke huyu alichotenda sio sawa.
Hatuwezi kuruhusu kukwepa kitendo alichofanya, alisema bi Engels.
Mwanamke huyo wa miaka 20 alisema: Ningefurahia sana iwapo angepelekwa jela.. hilo ndio lengo langu kwa sasa.
Bi Mugabe hajatoa tamko lolote kuhusu madai hayo.

Chanzo: BBC Swahili

No comments: