Advertisements

Tuesday, August 22, 2017

NEC yateuwa Madiwani 12 wanawake wa viti maalum

Kwa Mujibu wa Kifungu cha 86A (8) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) katika kikao chake cha kawaida kilichofanyika  tarehe 21 Agosti, 2017 na baada ya kushauriana na Vyama vya Siasa imewateua Madiwani Wanawake wa Viti Maalum kumi na wawili (12) kujaza nafasi wazi za Madiwani katika Halmashauri mbalimbali Tanzania Bara.
 
Madiwani Wanawake wa Viti Maalumu walioteuliwa ni kama ifuatavyo:

NA. JINA CHAMA HALMASHAURI
  1. 1
Ndugu Saida Idrisa Kiliula CUF Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

Ndugu Sophia Charokiwa Msangi CCM Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

Ndugu Shahara Selemani Nduvaruva CCM Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali

Ndugu Neema K. Nyangalilo CCM Halmashauri ya Manispaa ya Ilala

Ndugu Farida Zaharani Mohamed CCM Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

Ndugu Lucia Silanda Kadimu CCM Halmashauri ya Wilaya ya Tabora (Uyui)

Ndugu Amina Ramshi Mbaira CCM Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu

Ndugu Janeth John Kaaya CHADEMA Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Ndugu Sara Abdallah Katanga CHADEMA Halmashauri ya Manispaa ya Ilala

Ndugu Ikunda Massawe CHADEMA Halmashauri ya Wilaya ya Hai

Ndugu Tumaini Wilson Masaki CHADEMA Halmashauri ya Wilaya ya Siha

Ndugu Elizaberth Andrea Bayyo CHADEMA Halmashauri ya Mji wa Mbulu

Uteuzi huu umefanyika baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa ambaye kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 13(1) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292 alitaarifu Tume ya Taifa ya Uchaguzi uwepo wa nafasi hizo wazi.
 
Imetolewa  tarehe 21 Agosti, 2017
Kailima, R. K
 
MKURUGENZI WA UCHAGUZI

No comments: