Advertisements

Monday, August 7, 2017

RAIS DK.SHEIN AZUNGUMZA NA BODI YA BODI YA WAKURUGENZI BARAZA LA SANAA NA SENSA YA FILAMU

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein (katikati) alipokuwa akizungumza na  Uongozi wa Wizara ya Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo pamoja na Bodi ya Wakurugenzi Baraza la Sanaa na Sensa ya Filamu na Uongozi wa Baraza la Sanaa na Sensa ya Filamu katika kikao cha siku moja kilichofanyika leo Ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja,ambacho kimejadili mambo mbali mbali ya kiutendaji.
Katibu Mkuu wa  Wizara ya Habari,Utalii,Utamaduni na Michezo, Omar Hassan Omar (katikati) alipokuwa akifafanua jambo wakati wa kikao cha siku moja cha pamoja cha Wizara, Bodi ya Wakurugenzi Baraza la Sanaa na Sensa ya Filamu na Uongozi wa Baraza la Sanaa na Sensa ya Filamu kilichofanyika leo Ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja,chini ya Mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein. (Picha na Ikulu)

No comments: