Advertisements

Saturday, September 23, 2017

Diamond atua Afrika Kusini kwa Zari

By Mwandishi Wetu, Mwananchi

Ikiwa zimepita siku nne tangu mwanamuziki Diamond Platnumz akiri kumsaliti mpenzi wake Zari, hatimaye ametua nyumbani kwa mwanamke huyo nchini Afrika Kusini.

Leo saa 5.40 asubuhi mwanamuziki huyo aliposti video katika mtandao inayomuonyesha akicheza na mtoto wake wa kwanza, Latifah huku kwa mbali ikisikika sauti ya Zari.

Dada wa mwanamuziki huyo, Esmah Khan aliposti video hiyo katika mtandao wa Instagram: “Tuko na Tiffah na mamy tunaita raha ya mtoto apewe mapenzi kwa baba na mama jamani.”

Leo ilikuwa siku muhimu kwa Zari kwani anasherehekea siku yake ya kuzaliwa.

No comments: