Advertisements

Monday, November 20, 2017

DR NTUYABALIWE FOUNDATION YAHAMASISHA WANAFUNZI KUJIAMINI NA KUSOMA KWA BIDII

Mwalimu mkuu wa shule ya msingi ya Muungano, Esther Matowo(kushoto) akimkaribisha Mkurugenzi wa Dr.Ntuyabaliwe Foundation na Miss Tanzania 2000, Bi. Jacqueline Mengi mara alipowasili shuleni hapo leo kwenye siku ya maadhimisho ya siku mtoto Duniani.
Mkurugenzi wa Dr.Ntuyabaliwe Foundation na Miss Tanzania 2000, Bi. Jacqueline Mengi akizungumza na wanafunzi wa shule ya Msingi ya Muungano na Serengeti alipowatembelea katika maadhimisho ya Siku ya Mtoto Duniani yanayofanyika Novemba 20 ya kila mwaka.

Wanafunzi wamehamasishwa kujiamini na kusoma kwa bidii ili kujijengea msingi imara ya mafanikio katika maisha yao.
Hayo yamesemwa leo jijini Dar es salaam na Muasisi wa Dr. Ntuyabaliwe Foundation, Bi. Jacquiline Mengi alipowatembelea wanafunzi wa shule za msingi za Muungano na Serengeti zilizopo Manispaa ya Temeke, siku  ambayo duniani kote inaadhimishwa siku ya mtoto Duniani.

Akizungumza na wanafunzi hao Muasisi wa Dr. Ntuyabaliwe Foundation amesema ujumbe wake muhimu kwao wakati wa kuadhimisha siku ya mtoto Duniani ni kujiamini na kusoma kwa bidii, kwani ndiyo ufunguo wa mafanikio katika maisha
Akizungumza katika hafla hiyo Mkurugenzi wa Huduma ya simu kwa Mtoto ( C-SEMA)  Bw. Michael Marwa amewataka watoto kuripoti mara moja kwa njia ya simu vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa watoto ili wahusika wachukuliwe hatua.
Akitoa shukrani Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi ya Muungano, Esther Matowo amesema ujio wa Muasisi wa Taasisi ya Dr Ntubaliwe umewahamasisha  wanafunzi kujitambua na kujua wajibu wao. 

Hafla hiyo ilihudhuriwa pia na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke Salum Upunda, Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Serengeti Daud Sabai na walimu wa shule hizo mbili.
Mkurugenzi wa Huduma ya simu kwa Watoto( C-SEMA)  Bw. Michael Marwa akionesha namba ya huduma zinazotumika kuripoti mara moja kwa njia ya simu vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa watoto ili wahusika wachukuliwe hatua wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mtoto Duniani yanayofanyika Novemba 20 ya kila mwaka yaliyofanyika katika shuleni hapo.
Afisa Elimu na Ufundi manispaa ya Temeke, Salum B. Upunda aliyemwakilisha Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya watoto Duniani mara ya viongozi wa Dr. Ntuyabaliwe Foundation walipotembelea shuleni hapo leo.
Mwalimu mkuu wa shule ya msingi ya Muungano, Esther Matowo akitoa shukrani kwa uongozi wa Dr.Ntuyabaliwe Foundation kutembelea shuleni hapo na kuzungumza na wanafunzi wa shule hiyo wakati wa maadhimisho ya siku ya mtoto Duniani.

Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Serengeti na Muungano wakifuatilia mada wakati wa uongozi wa Dr.Ntuyabaliwe Foundation ulipotembelea shule hizo katika maadhimisho ya siku ya mtoto Duniani.
Mmoja wa wanafunzi akionesha kipaji cha kucheza wakati wa maadhimisho ya simu ya mtoto duniani.
Mkurugenzi wa Dr.Ntuyabaliwe Foundation na Miss Tanzania 2000, Bi. Jacqueline Mengi akiwa kwenye picha ya pamoja na wanafunzi wa shule ya msingi ya Serengeti na Muungano mara baada ya kuzungumza na wanafunzi hao wakati wa maadhimisho ya siku ya mtoto Duniani.
Mkurugenzi wa Dr.Ntuyabaliwe Foundation na Miss Tanzania 2000, Bi. Jacqueline Mengi  akiagana na wanafunzi wa shule ya msingi ya Serengeti na Muungano leo jijini Dar es Salaam.

No comments: