Advertisements

Friday, December 29, 2017

Waziri Mahiga apokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Uturuki nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Jamhuri ya Uturuki nchini, Mhe.Ali Dovutoglu. Makabidhiano hayo yamefanyika katika ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam tarehe 29 Desemba 2017. 
Mhe. Waziri Mahiga akizungumza na Mhe. Dovitoglu ambapo alimuhakikishia kumpa ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yake pamoja na kumpongeza kwa kuteuliwa kwake kwa awamu nyingine kuiwakilisha Jamhuri ya Uturuki nchini.

No comments: