Advertisements

Wednesday, February 28, 2018

DK MWANJELWA AANZA ZIARA YA KIKAZI MKOANI IRINGA, ATETA NA KINA MAMA WANAOJITEGEMEA 'SINGLE MOTHERS'


NAIBU Waziri wa Kilimo, Dk Mary Mwanjelwa akiongea machache na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Amina Masenza alipofika kwa utambulisho na kuanza ziara katika Mkoa huo Februari 23 2018. Pamoja naye (kushoto) Afisa Mtendaji Mkuu wa SAGCOT, Geoffrey Kirenga viongozi wa wasaidizi wake mkoani humo. (Imeandaliwa na Robert Okanda blogs)
NAIBU Waziri wa Kilimo, Dk Mary Mwanjelwa akisalimiana na mmoja wa wageni alipokutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Amina Masenza (kulia) alipofika kwa utambulisho na kuanza ziara katika Mkoa huo Februari 23 2018. Kulia kwa Naibu Waziri ni Afisa Mtendaji Mkuu wa SAGCOT, Geoffrey Kirenga.
NAIBU Waziri wa Kilimo, Dk Mary Mwanjelwa akiagana na Mkuu wa Mkoa, Mhe. Amina Masenza baada ya kufanya naye mazungumzo ofisini wakati wa kuanza kwa ziara yake mkoani humo. Kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa SAGCOT, Geoffrey.
NAIBU Waziri wa Kilimo, Dk Mary Mwanjelwa akikagua sehemu ya shamba lenye hekari 651 lililonunuliwa na Taasisi ya Ilula Programu 2013 wakati wa ziara yake mkoani Iringa Februari 23 2018. Katikati ni mwenyeji wao, Mhe Amina Masenza Mkuu wa Mkoa.
NAIBU Waziri wa Kilimo, Dk Mary Mwanjelwa akiwabadilishana mawazo na wakina mama wanajitegemea 'Single mothers' baada ya kukagua sehemu ya shamba lenye hekari 651 lililonunuliwa na Taasisi ya Ilula Programu 2013 mkoani Iringa kwa ajili ya kilimo cha biashara maalum kwa ajili yao, watoto yatima na wanafunzi wenye nia ya kukuza uelewa wa kilimo kutoka katika Wilaya ya Iringa hasa wa shule za primary na awali.

No comments: