Advertisements

Tuesday, February 13, 2018

KILOMBERO YAWAWEZESHA MAELFU YA WAZEE WASIOJIWEZA KATIKA HUDUMA ZA CHF ILIYOBORESHWA.

 Katibu Tawala wa mkoa wa Morogoro, Clifford Tandari  ( wapili  kushoto) akimkabidhi kadi ya bima ya afya ya Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) Iliyoboreshwa mzee  Petro Karubandika mkazi wa kata ya Mlimba , halmashauri ya wilaya ya Kilombero  wakati wa zoezi la ugawaji  kadi  hizo kwa wapatao  2,100 kutoka  vijiji 23 vya kata saba za Tarafa ya Mlimba na (  kushoto) ni  mkuu wa wilaya ya Kilombero, James Ihunyo na ( watatu kushoto) ni Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Kilombero, Dennis Londo.
 Katibu Tawala wa mkoa wa Morogoro, Clifford Tandari  ( wapili kushoto) akimkabidhi kadi ya bima ya afya ya Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) Iliyoboreshwa   Nelasi Nyingi , mkazi wa kata ya Mlimba , halmashauri ya wilaya ya Kilombero  wakati wa zoezi la ugawaji  kadi  hizo kwa wapatao  2,100 kutoka  vijiji 23 vya kata saba za Tarafa ya Mlimba (  kushoto ) ni mkuu wa wilaya ya Kilombero, James Ihunyo na ( watatu kushoto) ni Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Kilombero, Dennis Londo.
 Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri   ya Kilombero , Dennis Londo  ( kulia) akitoa maelezo mafupi ya mapango wa kuwakatia bima ya afya wazee  wasiojiweza kwa  Katibu tawala mkoa wa Morogoro, Clifford Tandari ( wapili kutoka kushoto) wakati wa  zoezi la ugawaji  kadi za CHF Iliyoboreshwa  kwa  wazee wapatao  2,100 wa  vijiji 23 vya kata saba za Tarafa ya Mlimba.
Baadhi ya wazee wa kata saba za tarafa ya Malimba , halmashauri ya wilaya ya Kilombero wakimsikiliza mgeni rasmi Katibu tawala mkoa wa Morogoro, Clifford Tandari  ( hayupo pichani) wakati wa  zoezi la ugawaji  kadi za CHF Iliyoboreshwa  kwa  wazee wapatao  2,100 wa  vijiji 23 vya kata saba za Tarafa ya Mlimba.  ( Picha na John Nditi).

Na John Nditi, Kilombero
HALMASHAURI ya wilaya ya Kilombero , mkoani Morogoro wamewakatia  kadi za   Mfuko wa Afya ya Jamii  (CHF ) iliyoboreshwa  wazee wasiojiweza zaidi ya 7,800 waliopo katika  kata  26  ili kuwawezesha kupata  huduma bora za matibabu katika vituo vya  Afya, Zahanati na hospitali na wategemezi wao.

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri  hiyo , Dennis Londo   alisema hayo  mbele ya  Katibu tawala mkoa wa Morogoro, Clifford Tandari, kabla ya zoezi la ugawaji  kadi za CHF Iliyoboreshwa  kwa baadhi ya wazee wapatao  2,100 kutoka  vijiji 23 vya kata saba za Tarafa ya Mlimba.

Londo  alisema   kuwa , hadi sasa  kiasi cha Sh milioni 13.3 zimetumika  kwa ajili ya mpango wa kuwakatia wazee wasiojiweza  bima  ya  afya ya CHF Iliyoboreshwa.

Hata hivyo alisema , halmashauri hiyo imejipanga  kuhakikisha wazee wanapatiwa bima ya Afya CHF iliyoboreshwa na lengo  ni  kuwafikia  wazee wasiojiweza  zaidi ya  15,000  katika kata zote 26.

“ Halmashauri ya wilaya hii imejipanga vyema na inatekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM  na miongoni mwa mam ohayo ni kundi la wazee wasiojiweza wamenufaka na huduma ya bima  ya afya” alisema Londo.

Naye Mwenyekiti wa halmashauri  hiyo , David Ligazio aliwataka watendaji wa vituo vya afya, zahanati na hospitali  ambaki madirisha ya wazee hayajaanzishwa waanzishe mara moja   ili  wazee hao wapate  unafuu wa huduma kulingana na lengo lililokusudiwa .

Kwa pande wake  mkuu wa wilaya ya Kilombero , James Ihunyo  alisema  , halmashauri hiyo inaendelea kufanya vizuri kutokana na  sehemu ya fedha zinazopatikana za   makusanyo ya ndani  kuelekezwa  kuboresha huduma za kijamii ikiwemo kuwakatia  bima  ya afya wazee wasiojiweza sambamba na kwa halmashauri ya mji Ifakara.

Awali  akisoma taarifa ya ugawaji wa kazi hizo ,  Ofisa Elimu Kata Kalengakelu,  Zainab Said  alisema,  wazee wasiojiweza walionufaika na mpango huo ni wa kutoka kwenye vijiji 23 vya  kata ya Chisano, Kalengakelu, Mlimba, Kamwene, Utengule , Masagati na Uchindile .

Akizungumza katika halfa hiyo katibu tawala wa mkoa huo, Tandari alizitaka halmashauri nyingine ndani ya mkoa huo  kuiga mfano wa halmashauri ya wilaya ya Kilombero  ili kuhakikisha wazee wote wanakuwa bima ya afya.


Nao baadhi ya wanufaika na mpango huowa CHF iliyoboreshwa ,Nelasi Nyingi  na Petro Karubandika kwa nyakati tofauti waliipongeza Serikali na uongozi wa halmashauri ya wilaya ya Kilombero  kwa kuwawezesha kuingizwa kunufaika na huduma za afya hasa ikizingatiwa wao wanahauwezo wa kifedha na wategemezi wao.

No comments: