Advertisements

Wednesday, February 28, 2018

NAIBU WAZIRI WA ARDHI MABULA AITAKA HALMASHAURI YA KARATU KUWAPA HATI ZA MADAI WADAIWA SUGU WA KODI YA ARDHI

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula akipokewa na Mkuu wa Wilaya ya Karatu Theresia Mahonga alipowasili katika wilaya hiyo kwa ziara ya kukagua mfumo wa ukusanyaji maduhuli ya kodi ya ardhi na kuzungumza na watumishi wa sekta ya ardhi.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula akizungumza na watumishi wa halmashahauri ya Wilaya ya Karatu mkoa wa Arusha.
Baadhi ya Watumishi wa halmashauri ya wilaya ya Karatu wakimsikiliza Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula.
Maofisa kutoka Wizara ya Ardhi na Kanda ya Kaskazini wakifuatilia mkutano baina ya Naibu Waziri wa Ardhi na watumishi wa halmashauri ya wilaya ya Karatu.
Sehemu ya watumishi wa halmashauri ya wilaya ya Karatu wakimsikiliza Naibu Waziri wa Ardhi Angelina Mabula.
Mkurugenzi Msaidizi Upimaji vijijini kutoka wizara ya Ardhi Huruma Lugalla akitoa ufafanuzi katika kikao baina ya Naibu Waziri wa Ardhi na Watumishi wa halmashauri ya wilaya ya Karatu.

No comments: