Advertisements

Wednesday, February 28, 2018

TCRA YASITISHA KURUSHA NYIMBO ZISIZOKUWA NA MAADILI


1 comment:

Anonymous said...

Kazi za Wasanii wa kiafrika hususani Tanzania, zinakufa kwa sababu ya "censorship" za kipuuzi. Hii ni "Political correctness" inayorudisha nyuma ufanisi wa wanamuziki na uwezo wao wa kujitangaza ulimwenguni. Kwa nini tunapoteza pesa za walipa kodi kuwa na Taasisi kama Basata, ambayo haina kazi yeyote muhimu ya kufanya, except to harass Tanzanian artists? Nimetembea mataifa mengi duniani ambako utazisikia Radio Stations na Night clubs zikipiga nyimbo za Diamond.."Waka Waka", "Hallelujah" n.k. Sisi wapenda muziki wa vijana wetu wa bongo tutaendelea kuwaunga mkono na kuzisikiliza nyimbo zote mlizozifunga. Tutatumia njia nyingine za kiteknolojia ambazo TCRA haina uwezo wa kuzifunga hapa bongo, ili kendelea kuburudika na BONGO FLAVA yetu. Bongo Flava siyo mali ya Serikali ya Awamu ya Tano, na haikuanzishwa kuifurahisha serikali au Wanasiasa wa Tanzania. Tuwaache vijana wakuze vipaji vyao, wapate ajira, na kulipa kodi ambazo zinalipa mishahara ya watumishi wa TCRA na Basata. Wadau wapenda muziki ndiyo wataamua kuzisikiliza hizi nyimbo au sivyo, na siyo serikali. Jamani, kwa nini tunarudi nyuma na kufuata fikra za kale za kikomunisti ambazo zimepitwa na wakati? Nakumbuka miaka ya Sabini hadi Tisaini nchi za Urusi, Eastern Europe, Cuba na Wachina ndiyo walikuwa wanaongoza kwa "censorship" wakidai kuwa ilikuwa ni kutekeleza maadili yao. Kwa nini Tanzania tunafanya hivyo katika karne hii ya Ishirini na moja? Serikali isipoteze muda na kutmia rasilimali zake kwenye vitu vidogo vidogo kama hivi, badala yake ifanye kazi ya kuujenga uchumi na kuleta maendeleo nchini.