"Sisi kama Tanzania tunaona ni ushirikiano mzuri sana ambao utavisaidia vyuo vyetu kupata fedha kwa ajili ya tafiti, lakini unafungua ukurasa mpya kwa ajili ya wanafunzi wanaotoka Tanzania kwenda kusoma kwenye vyuo vya Ufaransa, Ufaransa ni moja ya nchi duniani zenye mfumo mzuri sana wa elimu. "Kwa bahati mbaya sana (Watanzania) hawajanufaika na elimu ya Ufaransa kwa sababu pamoja na mambo mengine tatizo ni lugha, kwamba kile kinachotumika kule ni Kifaransa. Lakini pia ushirikiano huu utaumika kuimarisha mazingira ili wanafunzi wetu waweze kusoma Kifaransa lakini iwe ni rahisi kwao kuingia kwenye vyuo vya Ufaransa," alisema Ole Nasha.
Nae Balozi wa Ufaransa nchini, Frederic Clavier alisema ushirikiano huo utaboresha uhusiano uliopo sasa kati ya mataifa hayo mawili na muhimu zaidi ni kutoa elimu ambayo itawasaidia wanafunzi Watanzania hasa katika kipindi hiki ambacho Tanzania inaelekea katika uchumi wa kati. Alisema Ufaransa imekuwa ikipokea wanafunzi kutoka mataifa mbalimbali duniani ambao wanakwenda kusoma katika vyuo vikuu vya nchi hiyo na hivyo kuwataka Watanzania kutumia vyema ushirikiano huo ili waweze kusoma katika vyuo vya nchi hiyo na kupata fursa ya kufanya kazi katika mataifa zaidi ya 80 ambayo yanazungumza Kifaransa. "Ndoto imetia ya kuwepo kwa ushirikiano kati ya nchi hizi mbili katika elimu ya juu, kwa serikali yetu ni jambo muhimu sababu nchi zetu zinataka vijana kupata ujuzi ili kwenda mbele zaidi," alisema Clavier na kuongeza. "Ushirikiano huu utawezesha wanafunzi wa Tanzania kufahamu fursa zilizopo Ufaransa na kujua namna wanaweza kuzitumia, kwa sisi tayari tunao Wafaransa ambao wanajifunza Kiswahili katika vyuo mbalimbali hapa nchini." Na Rabi Hume, MO Dewji Blog
No comments:
Post a Comment