Advertisements

Thursday, March 1, 2018

WAJUMBE KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MASUALA YA UKIMWI NA MADAWA YA KULEVYA WATEMBELEA KONGA ZA WATU WANAOISHI NA VVU WILAYANI MBOZI MKOANI SONGWE.

 Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Capt. Chiku Galawa (kulia) akizungumza na Mjumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi na Madawa ya kulevya, Mhe. Venance Mwamoto (kushoto) na Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mhe. Dkt. Jasmine Tisekwa Bunga (katikati) pale kamati hiyo ilipomtembelea ofisini kwake kabla ya kuanza ziara ya kikazi ya kutembelea konga ya watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (VVU) katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, Mkoa wa Songwe.
 Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Capt. Chiku Galawa (kulia) akizungumza na Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi na Madawa ya kulevya, Baraza la Taifa la Watu Wanaoishi na VVU (NACOPHA) pamoja na JSI, iliyoongozwa na Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mhe. Dkt. Jasmine Tiisekwa Bunga (wa pili kushoto) kabla ya kuanza ziara ya kikazi ya kutembelea konga ya watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (VVU) katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, Mkoa wa Songwe.
 Mjumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi na Madawa ya kulevya, Mhe. Zaynab Vulu (kulia) akisalimiana na wana konga ya watu wanaoishi na VVU katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, Mkoa wa Songwe pale kamati hiyo ilipowatembelea katika ziara yake ya kikazi.

Makamu Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi na Madawa ya kulevya, Mhe. Dkt. Jasmine Tiisekwa Bunga (aliesimama)akizungumza na wana konga wanaoishi na VVU katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, Mkoa wa Songwe pale kamati hiyo ilipotembelea konga hiyo kwa ajili ya kuamasisha utumiaji wa dawa na jinsi ya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (VVU). (PICHA NA OFISI YA BUNGE)

No comments: