Advertisements

Tuesday, May 1, 2018

Ajiua kwa kunywa sumu kisa kuachwa na Mke

MWANAMUME mmoja mkazi wa Katoro mkoani Geita aliyetambulika kwa jina la Maganiko Nunda amejiua kwa kunywa sumu kufuatia mgogoro ulioibuka baina yake na mke wake siku hivi karibuni huku chanzo cha mgogoro huo kikidaiwa kuwa ni unywaji wa pombe kupindukia uliosababisha mkewe kumkimbia.

Akisimulia tukio hilo, mtoto wa marehemu amesema baada ya kwenda kumsalimia baba yake (marehemu) alimkuta ameshafariki huku akitokwa na povu mdomoni na puani.

Marehemu aliacha ujumbe wa barua wenye maneno yasemayo kuwa “…Kwa kuwa nimekuwa kero kwa familia yangu nimeamua kujiua…”

Aidha, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Mponjoli Mwabulambo amethibitisha kutokea kwa kifo hicho japo hakueleza ni aina gani ya sumu ambayo marehemu alitumia kujiua. Jeshi hilo linaendelea na upelelezi wa tukio hilo kabla ya kutoa taarifa kamili kwa umma.

No comments: