Kufuatia nyumba yake iliyopo Kisarawe kupigwa alama ya X huku akisemekana anatakiwa aibomoe kupisha upanuzi, Komedian maarufu nchini, Lucas Mhavile ‘Joti’ amefungukia tukio hilo ambalo limevuta hisia kwa mashabiki wake na Watanzania wengine waliotaka kujua undani wake.
Joti amesema; “Wanapanua barabara huku kwetu, lakini upanuzi huo wa barabara hauhusiani kabisa na ubomoaji wa nyumba, wengi wanajua nyumba yangu ndiyo inabomolewa, lakini sivyo kinachobomolewa ni ukuta tu.”
Nyumba ya Joti ni miongoni mwa nyumba zaidi ya 100 zilizopigwa X maeneo ya Kisarawe pamoja na Kibada ili kupisha upanuzi wa barabara.
No comments:
Post a Comment