Advertisements

Saturday, May 5, 2018

Joti Atoa Ufafanuzi Kuhusu Kubomolewa kwa Nyumba Yake.

Kufuatia  nyumba yake iliyopo Kisarawe kupigwa alama ya X huku akisemekana anatakiwa aibomoe kupisha upanuzi, Komedian maarufu nchini, Lucas Mhavile ‘Joti’ amefungukia tukio hilo ambalo limevuta hisia kwa mashabiki wake na Watanzania wengine waliotaka kujua undani wake.
Joti amesema; “Wanapanua barabara huku kwetu, lakini upanuzi huo wa barabara hauhusiani kabisa na ubomoaji wa nyumba, wengi wanajua nyumba yangu ndiyo inabomolewa, lakini sivyo kinachobomolewa ni ukuta tu.”

Eneo la Kisarawe na Kibada sio eneo la kwanza kwa Dar es Salaam kukukumbwa na adha ya bomoa bomoa, kabla ya hapo maeneo ya Kimara na Kinondoni Dar es Salaam nayo ilipita bomoa bomoa.

Nyumba ya Joti ni miongoni mwa nyumba zaidi ya 100 zilizopigwa X maeneo ya Kisarawe pamoja na Kibada ili kupisha upanuzi wa barabara.

No comments: