Advertisements

Friday, May 11, 2018

Mke wa Kafulila apata ajali ya gari

Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Jesca Kishoa amelazwa hospitali ya Bunge jijini Dodoma baada ya kupata ajali ya gari leo asubuhi Mei 11, 2018 wakati akienda bungeni.

“Hapa nimelazwa hospitali ya Bunge, nasikia maumivu katika mguu wa kulia lakini naendelea vizuri.

“Nimechomwa sindano ya kutuliza maumivu na ninaendelea vyema,” amesema Kishoa mke wa mbunge wa zamani wa Kigoma Kusini, David kafulila

Kuhusu mazingira ya ajali, Kishoa amesema;  “katika mataa ya pale Area D, taa zilivyoruhusu, yule wa mbele yangu hakuwa ameonyesha kama atakata kona, sasa alivyokata kwa ghafla, mimi kufunga breki kwa nguvu ikafeli, nikaigonga kwa nyuma.

No comments: