Advertisements

Sunday, May 6, 2018

Mwanafunzi wa Kidato cha Sita Ajinyonga

Siku moja kabla ya kuanza mitihani ya kidato cha sita, mtahiniwa wa Shule ya Sekondari Nyakato, Robert Masaba (21) amekufa ikidaiwa kuwa amejinyonga.

Kwa mujibu wa Baraza la Mitihani Tanzania (Necta) watahiniwa 87,643 wanatarajiwa kufanya mtihani wa kidato cha sita utakaoanza kesho Mei 7, 2018 hadi Mei 25, 2018.

Taarifa kutoka eneo la tukio zinadai Masaba amejinyonga usiku wa kuamkia leo Mei 6, 2018 kwenye mwembe akiwa Shule ya Sekondari Kahororo.

Masaba na wenzake walihamishiwa shuleni Kahororo zaidi ya mwaka mmoja uliopita baada ya sekondari ya Nyakato kuathiriwa na tetemeko la ardhi.

Mkuu wa Shule ya Kahororo, Omary Rugambaki amezungumzia tukio hilo akisema polisi wameshafika kwa uchunguzi.

No comments: