Advertisements

Monday, May 7, 2018

Queen Darlen Amtaka Harmonize Apunguze Uhuni Anamtesa Sarah

Mwanadada pekee kutoka katika kundi la wasafi, Queen Darlen amefunguka na kutoa ushauri kwa msanii mwenzake kutoka katika kundi hilo kwa kumtaka  Harmonize kupunguza tabia ya uhuni kwa sababu anamtesa sana sarah ambae ni mpenzi wake kwa sasa.

Queen Darlen amemtaka Harmonize kuacha kukata  tamaa katika kazi lakini amesmhauri kuwa inabidi apunguze kuwa na wanawake wengi na kutulia na mpenzi aliyenae kwa sasa amabe ni Sarah.

"Apunguze uhuni,atulie mtoto wa watu maskini ya Mungu mzungu yule  anampenda ila yeye mhuni mdogo wangu ,mhuni sana , mdogo wangu maisha ya uhuni sio mazuri anakuwa kama mfalme sulemani. aache hizo.

Hata hivyo kuna tetesi zimekuwa zikisambaa hivi karibuni kuhusu Harmonize kugombana na mpenzi wake huyo wa kizungu huku sababu kubwa ikiwa ni wivu wa mapenzi.

No comments: