Advertisements

Saturday, May 19, 2018

WAZIRI DKT. MWAKYEMBE AZINDUA COPA UMISSETA MJINI BUKOBA

 Waziri Mwakyembe akigawa vifaa vilivyotolewa na Coca-Cola kwa moja ya mwakilishi wa mmoja wa shule za sekondari.
 Waziri Mwakyembe akikagua moja ya timu wakati wa hafla ya uzinduzi.

 Wadau wa Umisseta katika picha ya pamoja na Waziri Mwakyembe.
 Waziri Mwakyembe akitoa hotuba ya ufunguzi wa mashindano hayo. Pembeni ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT) Said Kiganja.
 Waziri Mwakyembe akiongea na wanafunzi waliohudhuria.
Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Kagera,Mhandisi Richard Ruyango akiongea wakati wa hafla hiyo.
Waziri Mwakyembe akijiandaa kupiga penati  wakati wa uzinduzi huo. Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe amezindua mashindano ya shule za sekondari ya Copa Umisseta mjini Bukoba. Akizindua mshindano hayo mwishoni mwa wiki iliyopita katika Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba, Dkt. Mwakyembe ambaye alikuwa mgeni rasmi amesema michezo ni burudani, inaleta undugu, umoja na upendo hivyo h aina budi kuienzi siku zote. "Nawaomba vijana mpende michezo maana ni burudani na ilateta afya kwa watu wa rika zote, mkizingatia hivyo hakutakuwa na watu wenye magonjwa ya ajabu ajabu," amesema. Mashindano hayo yalipambwa na shamrashamra mbalimbali za michezo na burudani katika uwanja wa Kaitaba na kuhudhuriwa na viongozi wa serikali, wadau wa michezo na wanzi wa shule za sekondari na mgeni rasmi alikuwa ni Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe, aliyeambatana na Mkuu wa Wilaya ya Muleba, Mhandisi Richard Ruyango, aliyemwakilisha Mkuu wa mkoa wa Kagera pamoja na Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT) Said Kiganja.

No comments: