Kamanda wa polisi Mkoa wa Manyara Augustino Senga
Na Vero Ignatus , Manyara.
Mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jila la Josephine Peter (51)mkazi wa Mrara kata ya Mamire wilayani Babati ameuawa na watu wasiofahamika huku shingo yake ikikatwa na kitu chenye ncha kali.
Akizungumza leo june 21 Kamanda wa polisi mkoani Manyara Augustino Senga amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, amesema mwanamke huyo alifariki dunia juni 19 saa 4 usiku akiwa nyumbani kwake na mtu mmoja anashikiliwa na jeshi la polisi kwa uchunguzi zaidi kutokana na mauaji hayo.
Kamanda amesema kuwa hadi sasa chanzo cha mauaji hayo hakijafahamika kwani mwili wa marehemu umefanyiwa uchunguzi nakubainika kuwa hajabakwa kama watu wanavyozusha bali jeshi la polisi unaendelea na upelelezi wa tukio hilo la mauaji amesema kuwa ukikamilika taarifa kamili itatolewa
Mwili wa marehemu huyo umehifadhiwa kwenye hospitali ya mji wa Babati (Mrara)
No comments:
Post a Comment