Advertisements

Thursday, July 12, 2018

WAZIRI LUGOLA ATEMBELEA IDARA YA UHAMIAJI MAKAO MAKUU JIJINI DAR ES SALAAM


Kamishna Jenerali wa Uhamiaji,Dk. Anna Makakala akimkaribisha  Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola aliyefika Idara ya Uhamiaji jijini Dar es Salaam wakati wa ziara ya kikazi.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Ndani.
 Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akiangalia pasipoti ya kielektroniki inayotolewa na Idara ya Uhamiaji, alipotembelea Makao Makuu ya idara hiyo, jijini Dar es Salaam. Kulia ni Msimamizi wa chumba cha Uchapaji, Mrakibu Msaidizi, Samuel Gambadu.
 Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, akiongea na wananchi waliofika Makao Makuu ya Idara ya Uhamiaji, kupata huduma mbalimbali zinazotolewa na idara hiyo.jijini Dar es Salaam. 
 Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, akimuuliza swali mwananchi aliyefika Makao Makuu ya Idara ya Uhamiaji kupata huduma.Waziri Lugola yupo katika ziara ya kikazi.
 Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dk. Anna Makakala, akizungumza na Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, aliyefika Idara ya Uhamiaji,jijini Dar es Salaam,wakati wa ziara ya kikazi.

No comments: