Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akimpa maelekezo Mkuu wa Polisi Wilaya ya Chato, mkoani Geita, Alex Mukama (kushoto), kuhusu polisi wilayani humo wafanye kazi kwa weledi bila kunyanyasa wananchi. Waziri Lugola alifika Kituo cha Polisi Chato wilayani humo kusalimia pamoja na kupata taarifa ya utendaji kazi wa polisi, alipokua anatoka kuhani msiba wa dada wa Rais Dkt. John Magufuli, mjini Chato, leo. Kulia ni Mkuu wa Kituo hicho, Haruni Kasubo, na wapili kushoto, Diwani wa Kata ya Muungano, wilayani humo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto) akionyeshwa eneo la Kituo cha Polisi Chato na Mkuu wa Polisi Wilaya ya Chato, mkoani Geita, Alex Mukama (kushoto). Waziri Lugola alifika Kituo cha Polisi Chato wilayani humo kusalimia pamoja na kupata taarifa ya utendaji kazi wa polisi, alipokua anatoka kuhani msiba wa dada wa Rais Dkt. John Magufuli, mjini Chato, leo. Katikati ni Mkuu wa Kituo hicho, Haruni Kasubo.
No comments:
Post a Comment