Advertisements

Thursday, December 6, 2018

UNAIDS yaangalia namna ya kusaidia kituo cha Matumaini

Mkurugenzi Mkazi na Mwakilishi wa Shirika la Kupambana na UKIMWI la Umoja wa Mataifa (UNAIDS) nchini, Dk. Leo Zekeng akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili kwenye kijiji cha Matumaini kwa lengo la kutembelea kituoni hapo wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani. Kushoto ni mwenyeji wake Mkurugenzi wa Kijiji cha Matumaini, SR Maria Rosaria.
Mkurugenzi wa Kijiji cha Matumaini, SR Maria Rosaria akitoa maelezo kwa Mkurugenzi Mkazi na Mwakilishi wa Shirika la Kupambana na UKIMWI la Umoja wa Mataifa (UNAIDS) nchini, Dk. Leo Zekeng ya dawa mbalimbali wanazotumia kwa ajili ya watoto hao wanaolelewa kwenye kijiji cha Matumaini mjini Dodoma kinachoendeshwa na masista wa Kanisa Katoliki, Shirika la Masista Waabuduo Damu ya Yesu alipotembelea kituoni hapo wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani yaliyofanyika kitaifa mkoani humo.
Mkurugenzi Mkazi na Mwakilishi wa Shirika la Kupambana na UKIMWI la Umoja wa Mataifa (UNAIDS) nchini, Dk. Leo Zekeng akimkabidhi zawadi za ‘Pampers’ Mkurugenzi wa Kijiji cha Matumaini, SR Maria Rosaria alipotembelea kituo hicho kinachowalea watoto yatima wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani yaliyofanyika kitaifa mjini Dodoma.
Mkurugenzi Mkazi na Mwakilishi wa Shirika la Kupambana na UKIMWI la Umoja wa Mataifa (UNAIDS) nchini, Dk. Leo Zekeng akimsalimia mmoja wa watoto yatima anayelelewa kwenye kijiji cha Matumaini mjini Dodoma kinachoendeshwa na masista wa Kanisa Katoliki, Shirika la Masista Waabuduo Damu ya Yesu alipotembelea kituoni hapo wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani yaliyofanyika kitaifa mkoani humo.
Mkurugenzi wa Kijiji cha Matumaini, SR Maria Rosaria akimtambulisha Mkurugenzi Mkazi na Mwakilishi wa Shirika la Kupambana na UKIMWI la Umoja wa Mataifa (UNAIDS) nchini, Dk. Leo Zekeng kwa baadhi ya wafanyakazi wa kituo cha Afya cha kijiji cha Matumaini alipotembelea kituoni hapo kuwatia moyo wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani yaliyofanyika kitaifa mkoani humo.
Mkurugenzi Mkazi na Mwakilishi wa Shirika la Kupambana na UKIMWI la Umoja wa Mataifa (UNAIDS) nchini, Dk. Leo Zekeng akisalimiana na Daktari wa zamu wa kituo cha Afya cha kijiji cha Matumaini, Dr. John Zephania alipotembelea kituo hicho kinacholea watoto yatima kinachoendeshwa na masista wa Kanisa Katoliki, Shirika la Masista Waabuduo Damu ya Yesu wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani yaliyofanyika kitaifa mjini Dodoma.
Mkurugenzi Mkazi na Mwakilishi wa Shirika la Kupambana na UKIMWI la Umoja wa Mataifa (UNAIDS) nchini, Dk. Leo Zekeng akimbariki mtoto yatima anayelelewa kwenye kijiji cha Matumaini mjini Dodoma kinachoendeshwa na masista wa Kanisa Katoliki, Shirika la Masista Waabuduo Damu ya Yesu alipotembelea kituoni hapo wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani. Amembatana na Mkurugenzi wa Kijiji cha Matumaini, SR Maria Rosaria.
Mkurugenzi Mkazi na Mwakilishi wa Shirika la Kupambana na UKIMWI la Umoja wa Mataifa (UNAIDS) nchini, Dk. Leo Zekeng akiwa amembeba mmoja wa watoto yatima anayelelewa kwenye kijiji cha Matumaini mjini Dodoma kinachoendeshwa na masista wa Kanisa Katoliki, Shirika la Masista Waabuduo Damu ya Yesu alipotembelea kituoni hapo wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani yaliyofanyika kitaifa mjini Dodoma.


No comments: